HABARI YA KUJIFUNZA YA 10
WIMBO 31 Utembee Pamoja na Mungu!
Iga Namna ya Kufikiri ya Yehova na Yesu
“Kwa kuwa Kristo aliteseka katika mwili, ninyi pia mujipatie nguvu kwa muelekeo uleule wa akili.”—1 PE. 4:1.
WAZO KUBWA
Namna mutume Petro alijifunza namna ya kufikiri ya Yesu na namna na siye tunaweza kufanya vile.
1-2. Tunapaswa kumupenda Yehova namna gani, na namna gani Yesu alionyesha kama anamupenda Baba yake?
“UNAPASWA kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa nguvu zako zote na kwa akili yako yote.” (Lu. 10:27) Yesu alionyesha kama ile njo amri ya maana zaidi ya mu Sheria ya Musa. Tunapaswa kumupenda Yehova kwa moyo wetu, ni kusema namna tunajisikia na tamaa zetu zinapaswa kuonyesha kama tunamupenda. Pia tunapaswa kumupenda Yehova kwa nafsi yetu yote na nguvu yetu. Lakini, tunapaswa pia kumupenda Yehova kwa akili yetu, ni kusema namna yetu ya kufikiri inapaswa kuonyesha kama tunamupenda. Kusema kweli, hatuwezi kuelewa kabisa-kabisa namna yote ya kufikiri ya Yehova. Lakini tunaweza kuelewa zaidi namna yake ya kufikiri kwa kujifunza “akili ya Kristo,” juu Yesu aliiga kwa ukamili namna ya kufikiri ya Baba yake.—1 Ko. 2:16.
2 Yesu alimupenda Yehova kwa akili yake yote. Alijua mambo yenye Mungu alipenda afanye na aliazimia kuishi kulingana nayo, hata kama kufanya vile kungemuletea mateso. Juu Yesu alikazia akili kufanya mapenzi ya Baba yake, hakuacha jambo yoyote imuzuie kuifanya.
3. Mutume Petro alijifunza nini kutoka kwa Yesu, na alitia moyo Wakristo wenzake wafanye nini? (1 Petro 4:1)
3 Petro na mitume wengine walikuwa na pendeleo ya kupitisha wakati pamoya na Yesu na kujifunza namna yake ya kufikiri. Wakati Petro aliandika barua yake ya kwanza yenye iliongozwa na roho ya Mungu, alitia moyo Wakristo wajipatie nguvu kwa muelekeo uleule wa Kristo. a (Soma 1 Petro 4:1.) Wakati Petro aliandika “mujipatie nguvu,” alitumia maneno yenye mu luga ya kwanza-kwanza ilitumiwa juu ya kuzungumuzia askari mwenye anavala silaha ili kujitayarisha kwa ajili ya vita. Kwa hiyo, kama Wakristo wanaiga muelekeo wa akili wa Yesu ao namna yake ya kufikiri, watakuwa na silaha yenye nguvu yenye itawasaidia kupiganisha muelekeo wa kufanya zambi na vishawishi vya mu hii dunia yenye kutawaliwa na Shetani.—2 Ko. 10:3-5; Efe. 6:12.
4. Namna gani hii habari itatusaidia kufuata mashauri ya Petro?
4 Tutachunguza namna ya Yesu ya kufikiri na namna tunaweza kumuiga. Tutaona namna tunaweza (1) kuiga namna ya Yehova ya kufikiri, yenye itatusaidia tukuwe siye wote na akili moya, (2) namna tunaweza kuwa wanyenyekevu, na (3) namna tunaweza kuwa na akili ya muzuri kwa kumutegemea Yehova katika sala.
IGA NAMNA YA KUFIKIRI YA YEHOVA
5. Namna gani wakati fulani namna ya kufikiri ya Petro haikupatana na namna ya kufikiri ya Yehova?
5 Wakati fulani, namna ya kufikiri ya Petro haikupatana na namna ya kufikiri ya Yehova. Yesu aliambia mitume wake kama ataenda Yerusalemu, na kule viongozi wa dini watamukamata, atateswa, na kisha atauawa. (Mt. 16:21) Pengine ilikuwa nguvu kwa Petro kukubali kama Yehova ataruhusu Yesu, tumaini ya Israeli na Masiya mwenye aliahidiwa, auawe. (Mt. 16:16) Kwa hiyo Petro alimubeba Yesu pembeni na akamuambia hivi: “Jitendee kwa fazili, Bwana; mambo hayo hayatakupata hata kidogo.” (Mt. 16:22) Petro hakukuwa na mawazo sawa ya Yehova juu ya ile jambo, njo maana mawazo yake haikupatana na mawazo ya Yesu.
6. Yesu alionyesha namna gani kama namna yake ya kufikiri ilipatana na namna ya kufikiri ya Yehova?
6 Namna ya Yesu ya kufikiri ilipatana kabisa na namna ya kufikiri ya Baba yake wa mbinguni. Yesu alimuambia hivi Petro: “Pita nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa sababu unawaza mawazo ya wanadamu.” (Mt. 16:23) Pengine Petro alikuwa na nia ya muzuri, lakini Yesu alikatala shauri yake. Ile inatufundisha jambo ya maana. Mapenzi ya Yehova haikukuwa Yesu akwepe mateso. Mu ile hali, Petro alijifunza somo ya maana sana kuhusu namna ya kupatanisha mawazo yake na mawazo ya Yehova.
7. Namna gani Petro alifikia kupatanisha namna yake ya kufikiri na namna ya kufikiri ya Yehova? (Ona picha .)
7 Petro alifikia kuonyesha kama alipenda kupatanisha namna yake ya kufikiri na namna ya kufikiri ya Yehova. Wakati ulifika juu Batu ya Mataifa bajiunge pia na batu ya Mungu. Petro alipewa mugao wa kuhubiria Kornelio, mwenye alikuwa kati ya Batu ya Mataifa ba kwanza-kwanza benye balifikia kuwa Bakristo. Wayahudi hawakukuwa najiunga na Batu ya Mataifa, njo maana iliomba Petro atayarishwe mbele ya kutimiza mugao wake. Wakati Petro alielewa mapenzi ya Mungu juu ya ile jambo, alibadilisha mawazo yake. Kwa hiyo wakati Mungu alimutuma, alienda “bila kupinga.” (Mdo. 10:28, 29) Alihubiria Kornelio na batu ya nyumba yake, na bote bakabatizwa.—Mdo. 10:21-23, 34, 35, 44-48.
Petro iko naingia mu nyumba ya Kornelio (Ona fungu ya 7)
8. Namna gani tunaweza kuonyesha kama namna yetu ya kufikiri inapatana na namna ya Yehova ya kufikiri? (1 Petro 3:8 na maelezo ya chini)
8 Kisha miaka, Petro alitia moyo Wakristo wenzake ‘wakuwe na umoja wa akili.’ (Soma 1 Petro 3:8 na maelezo ya chini.) Juu tuko batu ya Yehova, tunaweza kuwa na namna moya ya kufikiri kama tunaiga namna ya Yehova ya kufikiri yenye kuonyeshwa mu Neno yake. Kwa mufano, Yesu alishauria wafuasi wake watie Ufalme fasi ya kwanza mu maisha yao. (Mt. 6:33) Tuseme muhubiri fulani mu kutaniko yenu anaamua kuingia mu aina fulani ya utumishi wa wakati wote. Kuliko kumuambia asijihangaishe, tunaweza kumupongeza juu ya uamuzi wake na kumutegemeza.
UKUWE MUNYENYEKEVU
9-10. Namna gani Yesu alionyesha unyenyekevu wa ajabu?
9 Usiku mbele Yesu auawe, alifundisha Petro na mitume wengine somo ya maana sana juu ya unyenyekevu. Yesu alituma Petro na Yohana waende kufanya matayarisho juu ya chakula ya mwisho yenye angekula pamoya nao. Inawezekana mu matayarisho, walihakikisha kama kuko beseni na nguo ya kupanguzia juu wageni wanawishwe migulu mbele ya kula. Lakini nani njo angefanya ile kazi ya hali chini?
10 Bila kusita Yesu alionyesha unyenyekevu wa ajabu sana. Alifanya jambo yenye kwa kawaida mutumishi njo anafanyaka. Ile ilishangaza sana mitume wake. Yesu alitosha nguo yake ya inje, akajifunga mu kiuno nguo ya kupanguzia, akatia mayi mu beseni, na akaanza kunawisha mitume migulu. (Yoh. 13:4, 5) Inawezekana ilikamata wakati juu ya kunawisha migulu ya mitume wote 12, kutia ndani Yuda mwenye alifikia kumusaliti. Lakini kwa unyenyekevu Yesu alifanya ile kazi. Kisha Yesu akaambia mitume hivi: “Je, munaelewa jambo lenye nimewafanyia? Ninyi munaniita, ‘Mwalimu,’ na, ‘Bwana,’ na munasema kweli, kwa maana ni vile niko. Kwa hiyo, kama mimi mwenye ni Bwana na Mwalimu, niliwanawisha ninyi miguu, ninyi pia munapaswa kunawishana miguu.”—Yoh. 13:12-14.
Unyenyekevu wa kweli . . . unatoka ndani kabisa ya moyo
11. Namna gani Petro alionyesha kama alijifunza kuwa munyenyekevu? (1 Petro 5:5) (Ona pia picha.)
11 Petro alijifunza kupitia unyenyekevu wa Yesu. Kisha Yesu kurudia mbinguni, Petro alifanya muujiza fulani: aliponyesha mwanaume mwenye alikuwa kilema tangu kuzaliwa. (Mdo. 1:8, 9; 3:2, 6-8) Bila shaka ile ilifanya batu mingi bamuzunguke. (Mdo. 3:11) Petro hakujisifu hata kama alikomalia mu desturi yenye batu balipenda kusifiwa na kujulikana. Kwa unyenyekevu alionyesha kama ni Yehova na Yesu njo banastahili sifa, alisema hivi: “Kupitia jina lake [Yesu], na kupitia imani yetu katika jina lake, mwanaume huyu mwenye munaona na munamujua, amefanywa akuwe na nguvu.” (Mdo. 3:12-16) Maneno yenye Petro alitumia mu barua yenye aliandikia Wakristo yenye inaonyesha juu ya nini ni jambo ya maana kukomalisha sifa ya unyenyekevu, inaweza kutukumbusha namna Yesu alijifunga mu kiuno nguo na kusafisha migulu ya mitume wake.—Soma 1 Petro 5:5.
Kisha Petro kufanya muujiza, kwa unyenyekevu alionyesha kama Yehova na Yesu njo wanastahili sifa. Na siye pia tunaweza kuonyesha kama tuko wanyenyekevu kwa kufanya mambo ya muzuri bila kutazamia wengine watuone, watusifu ao watupatie jambo fulani (Ona fungu ya 11-12)
12. Kama Petro namna gani tunaweza kuendelea kukomalisha sifa ya unyenyekevu?
12 Tunaweza kufuata mufano wa Petro kwa kujikaza kukomalisha sifa ya unyenyekevu. Kumbuka kama unyenyekevu wa kweli hauonekane tu mu maneno. Maneno “unyenyekevu wa akili” yenye Petro alitumia juu ya kuzungumuzia unyenyekevu, inaonyesha kama ile sifa inatoka ndani kabisa ya moyo. Tunatumikia bengine juu tunamupenda Yehova na tunapenda batu, haiko juu tunapenda batuone. Kama tunafanya yetu yote juu ya kumutumikia Yehova na kutumikia bandugu yetu kwa furaha, ikuwe bengine banaona ao hapana, tunaonyesha kama tuko banyenyekevu.—Mt. 6:1-4.
UKUWE NA “AKILI YA MUZURI”
13. Kuwa na “akili ya muzuri” maana yake nini?
13 Kuwa na “akili ya muzuri” maana yake nini? (1 Pe. 4:7) Mukristo mwenye iko na akili ya muzuri anafanya yake yote juu ya kukamata maamuzi ya muzuri yenye inapatana na namna ya kufikiri ya Yehova. Mukristo wa vile anajua kama uhusiano wake pamoya na Yehova njo wa maana zaidi mu maisha. Iko mwenye usawaziko na anakubali kama hajue mambo yote. Anaonyesha kama anamutegemea Mungu kwa kusali kwake kwa ukawaida na kwa unyenyekevu. b
14. Namna gani Petro alishindwa kumutegemea Yehova?
14 Usiku wa mwisho mbele Yesu auawe, alionya hivi banafunzi yake: “Ninyi wote mutakwazika usiku huu” Petro alijibia hivi kwa uhakika: “Hata kama wengine wote wanakwazika kwa sababu ya mambo yenye yatakupata, mimi sitakwazika hata kidogo!” Ile usiku Yesu alishauria banafunzi yake fulani hivi: “Muendelee kukesha na kusali bila kuacha.” (Mt. 26:31, 33, 41) Kama Petro angefuata ile shauri, angekuwa na uhodari wa kukubali kama alikuwa mwanafunzi wa Yesu. Kuliko kufanya vile, Petro alimukana Bwana wake, na alifikia kuhuzunika sana juu ya ile.—Mt. 26:69-75.
15. Usiku mbele Yesu akufe, namna gani alionyesha kama aliendelea kuwa na akili ya muzuri?
15 Yesu alimutegemea kabisa Yehova. Hata kama alikuwa mukamilifu, alisali mara mingi. Ile ilimupatia uhodari wa kuishi kulingana na mapenzi ya Yehova. (Mt. 26:39, 42, 44; Yoh. 18:4, 5) Bila shaka kuona namna Yesu alisali mara mingi, ni jambo yenye Petro alikumbuka mu maisha yake yote.
16. Petro alionyesha namna gani kama alifikia kuwa na akili ya muzuri? (1 Petro 4:7)
16 Kisha wakati, Petro alijifunza kumutegemea Yehova kupitia sala. Yesu mwenye alikuwa sasa amefufuliwa alihakikishia Petro na mitume wengine kama watapokea roho takatifu juu waweze kutimiza kazi ya kuhubiri yenye aliwapatia. Lakini Yesu aliwaambia wabakie Yerusalemu mupaka wakati atawapatia roho takatifu. (Lu. 24:49; Mdo. 1:4, 5) Petro alifanya nini wakati walikuwa nangoya roho takatifu? Petro na Wakristo wenzake “waliendelea kusali bila kuacha.” (Mdo. 1:13, 14) Mu barua yake ya kwanza, Petro alitia moyo Wakristo wenzake wakuwe na akili ya muzuri na waendelee kumutegemea Yehova kwa kusali. (Soma 1 Petro 4:7.) Petro alijifunza kumutegemea Yehova na alitia nguvu bandugu na badada yake.—Gal. 2:9.
17. Hata kama tuko na uwezo gani tunapaswa kuendelea kufanya nini? (Ona pia picha.)
17 Juu tukuwe na akili ya muzuri, tunapaswa kusali kwa Yehova kwa ukawaida. Tunajua kama tunapaswa kuendelea kusali kwa Yehova hata kama tuko na uwezo mbalimbali. Kwa hiyo, tunasali kwa Yehova juu ya kumuomba muongozo na tunatumainia kama yeye njo anajua mambo yenye itatuletea faida; ni muzuri tufanye vile zaidi sana wakati tunatafuta kukamata maamuzi ya maana.
Petro alijifunza kumutegemea Yehova kwa kusali. Siye pia tunaweza kuwa na akili ya muzuri kwa kusali kwa Yehova atusaidie, zaidi sana wakati tunataka kukamata maamuzi ya maana (Ona fungu ya 17) c
18. Namna gani tunaweza kupatanisha namna yetu ya kufikiri na namna ya Yehova ya kufikiri?
18 Tuko wenye shukrani sana juu Yehova alituumba na uwezo wa kuonyesha sifa zake. (Mwa. 1:26) Ni kweli kama hatuwezi kumuiga Yehova kwa ukamili. (Isa. 55:9) Lakini kama Petro, tunaweza kupatanisha namna yetu ya kufikiri na namna ya kufikiri ya Yehova. Tuendelee basi kufanya vile kwa kuiga namna ya kufikiri ya Yehova, kwa kuwa wanyenyekevu, na kuwa na akili ya muzuri.
WIMBO 30 Baba Yangu, Mungu Wangu, na Rafiki Yangu
a “Muelekeo wa akili,” yenye kuwa mu 1 Petro 4:1, inaweza pia kutafsiriwa “mutazamo,” ao “kufikiri.”
b Juu ya kuelewa muzuri maana ya kuwa na akili ya muzuri, ao kuwa na hali ya muzuri ya kiroho, ku jw.org ao ku JW Library® ona habari “2 Timotheo 1:7—‘Mungu Hakutupa Roho ya Woga,’” mu sehemu “Mistari ya Biblia Yafafanuliwa.”
c MAFASIRIO YA PICHA: Dada iko nasali kimya-kimya wakati iko nangoya wamuulize maulizo juu ya kazi.