HABARI YA KUJIFUNZA YA 25

WIMBO 96 Biblia Ni Kitabu ya Maana Sana

Maneno ya Unabii ya Yakobo Inatufundisha Nini?—Sehemu ya 2

Maneno ya Unabii ya Yakobo Inatufundisha Nini?—Sehemu ya 2

“Alipatia kila mumoja wao baraka yenye kumustahili.”MWA. 49:28.

WAZO KUBWA

Mambo yenye tunajifunza wakati tunachunguza mambo yenye Yakobo aliambia batoto yake bengine munane mbele akufe.

1. Tutazungumuzia nini mu hii habari?

 BATOTO ya Yakobo banamuzunguka. Banasikiliza kwa uangalifu mambo yenye iko naambia kila mutu. Sawa vile tuliona mu habari yenye ilitangulia, pengine mambo yenye Yakobo aliambia Rubeni, Simeoni, Lawi na Yuda ilibashangaza sana. Kwa hiyo pengine biko najiuliza ataambia nini batoto yake bengine munane. Mu hii habari tutaona mambo yenye Yakobo aliambia Zabuloni, Isakari, Dani, Gadi, Asheri, Naftali, Yosefu, na Benyamini. a Kisha tutaona ile mambo inatufundisha nini.

ZABULONI

2. Yakobo alitabiri nini juu ya Zabuloni na namna gani ile maneno ilitimia? (Mwanzo 49:13) (Ona pia  kisanduku.)

2 Soma Mwanzo 49:13. Yakobo alisema kama bazao ya Zabuloni bangeishi pembeni ya bahari, ni kusema kaskazini mu Inchi ya Ahadi. Ule unabii ulitimia kisha zaidi ya miaka 200, wakati Bazabuloni balipewa uriti. Eneo yenye baliriti ilikuwa katikati ya bahari ya Galilaya na bahari ya Mediterania. Njo maana Musa alitabiri hivi juu yao: “Shangilia, Ee Zabuloni, wakati unatoka inje.” (Kum. 33:18) Pengine ile maneno ya Musa ilimaanisha kama, juu Bazabuloni balikuwa katikati ya bahari mbili, ingekuwa mwepesi kwao kufanya biashara pamoya na batu ba kutoka mu maeneo ingine. Ikuwe mambo ilikuwa vile ao hapana, Bazabuloni balikuwa na sababu ya kufurahi.

3. Nini njo inaweza kutusaidia tutosheke?

3 Tunajifunza nini? Tuko na sababu za mingi za kuwa na furaha ikuwe tunaishi wapi ao tuko mu hali gani. Lakini juu tuendelee kuwa na furaha tunapaswa kutosheka na bienye tuko nabyo. (Zb. 16:6; 24:5) Ni mwepesi kukazia akili mambo yenye hatuna kuliko kuona mambo ya muzuri yenye tuko nayo. Njo maana tunapaswa kujikaza kuona mambo ya muzuri yenye tuko nayo na kufurahia maisha.—Gal. 6:4.

ISAKARI

4. Yakobo alitabiri nini juu ya Isakari na ile maneno ilitimia namna gani? (Mwanzo 49:14, 15) (Ona pia  kisanduku.)

4 Soma Mwanzo 49:14, 15. Yakobo anasifu Isakari juu anatumikaka sana, anamulinganisha na punda, munyama mwenye nguvu mwenye anabebaka mizigo ya buzito. Tena Yakobo anasema kama Isakari atariti eneo ya muzuri. Ile maneno ya Yakobo ilitimia wakati bazao ya Isakari balipewa eneo yenye mboleo karibu na muto Yordani. (Yos. 19:22) Balitumika sana juu ya kulima eneo yabo na balitumika pia sana juu ya kusaidia bengine. (1 Fa. 4:7, 17) Kwa mufano, wakati muamuzi Baraka na nabii mwanamuke Debora baliomba Baisraeli basaidie kupigana na Sisera, kabila ya Isakari ilijitolea na ilisaidia ku pigania taifa mu vita zingine.—Amu. 5:15

5. Juu ya nini tunapaswa kujikaza kutumika sana?

5 Tunajifunza nini? Yehova anafurahia kazi ya nguvu yenye tuko nafanya mu utumishi wake, sawa vile tu alifurahia kazi ya nguvu ya kabila ya Isakari. (Muh. 2:24) Kwa mufano, fikiria bandungu benye banatumikaka sana juu ya kusaidia kutaniko. (1 Ti. 3:1) Habaendake kupigana vita, lakini banajitoaka sana juu ya kulinda batu ya Mungu na kubasaidia baendelee kuwa na hali ya muzuri ya kiroho. (1 Ko. 5:1, 5; Yud. 17-23) Tena banatumikaka sana juu ya kutayarisha na kutoa hotuba zenye zinatia nguvu kutaniko.—1 Ti. 5:17.

DANI

6. Kabila ya Dani ilipewe kazi gani? (Mwanzo 49:17, 18) (Ona pia  kisanduku.)

6 Soma Mwanzo 49:17, 18. Yakobo analinganisha Dani na nyoka mwenye analuma wanyama wakubwa kumupita, sawa vile farasi wa vita. Kabila ya Dani ilikuwa tayari kushambulia maadui wa Israeli. Wakati Baisraeli balikuwa mu safari ya kuenda mu Inchi ya Ahadi, kabila ya Dani ililinda taifa. Batu ya kabila ya Dani ‘balikuwa kikundi cha nyuma cha kulinda kambi.’ (Hes. 10:25) Ile ilikuwa kazi ya maana sana, hata kama Baisraeli bengine habakuona mambo yenye kabila ya Dani ilikuwa nafanya nyuma yao.

7. Tunapaswa kukumbuka nini juu ya mambo yote yenye tunafanya mu utumishi wa Yehova?

7 Tunajifunza nini? Ulishaka kufanya kazi fulani lakini bengine habakuona mambo yenye ulifanya? Pengine ulisaidia kusafisha na kutunza Jumba ya Ufalme, ulijitolea kutumika ku mukusanyiko ao ulifanya kazi ingine. Ujue kama ulifanya muzuri sana na ukumbuke kama Yehova anaona na anafurahia mambo yote yenye uko namufanyia. Anafurahi sana wakati unamutumikia juu unamupenda kabisa, hapana juu unapenda bengine bakusifu.—Mt. 6:1-4.

GADI

8. Juu ya nini ilikuwa mwepesi kwa maadui wa Israeli kushambulia kabila ya Gadi? (Mwanzo 49:19) (Ona pia  kisanduku.)

8 Soma Mwanzo 49:19. Yakobo alitabiri kama kikundi ya wanyanganyi kingeshambulia Gadi. Ile maneno ilitimia kisha zaidi ya miaka 200 wakati kabila ya Gadi ilipewa eneo yenye ilikuwa mashariki ya Muto Yordani, eneo yenye ilikuwa ku mipaka na maadui wa Israeli. Kwa hiyo, ilikuwa mwepesi kwa maadui kuwashambulia. Lakini batu ba kabila ya Gadi balipenda kuishi pale juu kulikuwa mayani mingi yenye ingekulisha wanyama wao wa kufugwa. (Hes. 32:1, 5) Batu ya kabila ya Gadi balikuwa hodari na balitumainia kama Yehova atabasaidia kulinda eneo yenye alibapatia na atabasaidia bapiganishe wanyanganyi. Na hata, kwa miaka mingi balituma maaskari waende kusaidia Baisraeli kukamata sehemu ya Inchi ya Ahadi yenye ilikuwa ngambo ingine ya Yordani. (Hes. 32:16-19) Balimutumainia Yehova, balikuwa hakika kama Yehova atalinda bibi zao na batoto yao wakati banaume balienda kupigana vita. Yehova alibabariki juu balikuwa hodari na balikuwa tayari kusaidia bengine, hata wakati haikukuwa mwepesi.—Yos. 22:1-4.

9. Kama tunamutumainia Yehova, tutakuwa tayari kukamata maamuzi gani?

9 Tunajifunza nini? Juu tuendelee kumutumikia Yehova mu hali ya nguvu, tunapaswa kuendelea kumutumainia. (Zb. 37:3) Leo batu mingi banamutumainia Yehova. Njo maana banajitoa juu ya kusaidia mu kazi mbalimbali za ujenzi, kuenda kutumikia kwenye kuko lazima kubwa ya bahubiri ao kutumikia migao ingine mu kazi ya Yehova. Banafanya ile mambo yote juu biko hakika kama Yehova atabahangaikia.—Zb. 23:1.

ASHERI

10. Batu ya kabila ya Asheri habakufanya nini? (Mwanzo 49:20) (Ona pia  kisanduku.)

10 Soma Mwanzo 49:20. Yakobo alitabiri kama kabila ya Asheri ingekuwa tajiri. Vile njo mambo ilikuwa. Mu Israeli, eneo ya kabila ya Asheri ilikuwa kati ya maeneo kwenye chakula ya mingi ilikuwa natoka. (Kum. 33:24) Tena, eneo yabo ilikuwa pembeni ya bahari ya Mediterania na ni mu ile eneo njo mulikuwa bandari ya Sidoni yenye ilikuwa na utajiri. Lakini, kabila ya Asheri ilishindwa kufukuza Bakanaani mu ile eneo. (Amu. 1:31, 32) Juu balichochewa na tabia za mubaya za Bakanaani na juu balikuwa matajiri, pengine ile mambo ilifanya bapunguze bidii yabo ya kumutumikia Yehova. Kwa mufano, wakati Baraka aliomba Baisraeli bamusaidie kupiganisha majeshi ya Bakanaani, batu ya kabila ya Asheri habakujitoa kusaidia. Kwa hiyo, habakuona mambo ya ajabu yenye Yehova alifanya juu ya kusaidia Baisraeli kwa kushinda ile vita “pembeni ya maji ya Megido.” (Amu. 5:19-21) Na inawezekana balisikia haya sana wakati balisikia hii maneno yenye Baraka na Debora balisema mu wimbo wa ushindi: “Asheri alikaa bila kufanya kazi pembeni ya bahari.”—Amu. 5:17.

11. Juu ya nini hatupaswe kuhangaikia sana bitu ya kimwili?

11 Tunajifunza nini? Tunapenda kumutumikia Yehova kwa moyo wetu wote. Juu tufanye vile, tunapaswa kuepuka mawazo ya ulimwengu kuhusu bitu ya kimwili. (Mez. 18:11) Tunajua kama kumutumikia Yehova njo jambo ya maana sana kupita kuwa na makuta. (Muh. 7:12; Ebr. 13:5) Hatuache bitu ya kimwili bituzuie kumutumikia Mungu. Lakini tunatoa wakati wetu na nguvu yetu juu ya kumutumikia Yehova kwa moyo wote leo, juu tunajua kama tukiendelea kuwa baaminifu, Yehova atatubariki na kutupatia maisha ya muzuri na hatutakosa kitu.—Zb. 4:8.

NAFTALI

12. Inawezekana mambo yenye Yakobo alisema juu ya Naftali ilitimia namna gani? (Mwanzo 49:21) (Ona pia  kisanduku.)

12 Soma Mwanzo 49:21. Yakobo alitabiri kama Naftali atasema “maneno yenye kupendeza.” (Mwa. 49:21) Inawezekana ule unabii ulitimia wakati wa utumishi wa Yesu. Yesu mwenye alikuwa mwalimu muzuri, alipitisha wakati mingi mu kapernaumu yenye ilikuwa mu eneo ya kabila ya Naftali. Njo maana baliita Kapernaumu “muji wake mwenyewe.” (Mt. 4:13; 9:1; Yoh. 7:46) Na Isaya alitabiri kama Yesu atakuwa kama “mwangaza mukubwa” kwa watu wa Zabuloni na Naftali. (Isa. 9:1, 2) Kupitia mafundisho yake, Yesu alikuwa “mwangaza wa kweli wenye unaangazia watu wa kila namna.”—Yoh. 1:9.

13. Tunaweza kufanya nini juu maneno yetu imufurahishe Yehova?

13 Tunajifunza nini? Yehova anahangaikia mambo yenye tunasema na namna tunaisema. Namna gani tunaweza kusema “maneno yenye kupendeza” yenye inamufurahisha Yehova? Kwanza, tunapaswa kusema kweli. (Zb. 15:1, 2) Pia, tunaweza kutia bengine moyo kwa kuwa tayari kubapongeza na kuepuka kubasema mubaya ao kunungunika-nungunika. (Efe. 4:29) Tunaweza pia kukomalisha ufundi wetu wa kuanzisha mazungumuzo na batu juu tuweze kubahubiria habari njema.

YOSEFU

14. Fasiria namna maneno yenye Yakobo alisema juu ya Yosefu ilitimia. (Mwanzo 49:22, 26) (Ona pia  kisanduku.)

14 Soma Mwanzo 49:22, 26. Yakobo alifurahia sana mutoto yake Yosefu. Yehova alimuchagua kati ya “ndugu zake” juu atimize mugao wa maana. Yakobo alimuita “chipukizi la muti wenye kuzaa matunda.” Yakobo mwenyewe njo alikuwa muti, na Yosefu njo alikuwa chipukizi ao tawi. Yosefu njo alikuwa mutoto wa kwanza wa Raheli, bibi mupendwa wa Yakobo. Yakobo alisema kama Yosefu njo atapata sehemu mbili ya uriti yenye Rubeni muzaliwa wa kwanza wa Lea alipoteza. (Mwa. 48:5, 6; 1 Ny. 5:1, 2) Ule unabii ulitimia wakati Efraimu na Manase, batoto bawili ba Yosefu, balifikia kuwa makabila mbili tofauti ya Israeli na kila kabila ikapewa uriti.—Mwa. 49:25; Yos. 14:4.

15. Yosefu alifanya nini wakati balimutendea mubaya?

15 Yakobo alisema pia kama bapiga-mishale ‘balimutupia [Yosefu] mishale na baliendelea kumuwekea chuki.’ (Mwa. 49:23) Bale bapiga-mishale ni bandugu yake benye balimusikilia wivu. Balimutendea mubaya, na ni juu yabo njo mambo mingi ya mubaya ilimufikia Yosefu. Lakini Yosefu hakuchukia bandugu yake na hakumukasirikia Yehova. Yakobo alisema hivi juu ya Yosefu: “Upinde wake [Yosefu] ulibakia mahali pake, na mikono yake iliendelea kuwa na nguvu na myepesi.” (Mwa. 49:24) Yosefu aliendelea kumutumikia Yehova mu magumu yake yote, alisamehe bandugu yake, na alibatendea muzuri. (Mwa. 47:11, 12) Magumu yenye alipitia ilifanya akuwe mutu muzuri zaidi. (Zb. 105:17-19) Njo maana Yehova alimutumikisha juu ya kufanya mambo mingi ya ajabu.

16. Tunaweza kumuiga Yosefu namna gani wakati tuko na magumu?

16 Tunajifunza nini? Tusiache hata siku moya magumu itutenganishe na Yehova ao na baabudu benzetu. Tukumbuke kama Yehova anaweza kuruhusu magumu itufikie. (Ebr. 12:7, maelezo ya chini.) Ile magumu inaweza kuwa kama mazoezi yenye itatusaidia kuwa na imani ya nguvu na kukomalisha sifa za Kikristo sawa vile rehema na kusamehe bengine. (Ebr. 12:11) Tukuwe hakika kama, sawa vile Yehova alibariki Yosefu, na siye atatubariki juu ya uvumilivu wetu.

BENYAMINI

17. Mambo yenye Yakobo alitabiri juu ya Benyamini ilitimia namna gani? (Mwanzo 49:27) (Ona pia  kisanduku.)

17 Soma Mwanzo 49:27. Yakobo alitabiri kama bazao ya Benyamini batakuwa bapiganaji benye nguvu sawa vile imbwa wa pori. (Amu. 20:15, 16; 1 Ny. 12:2) “Asubui,” ni kusema ku mwanzo wa utawala wa Israeli, Sauli mufalme wa kwanza wa Israeli alitoka mu kabila ya Benyamini. Sauli alipigana kwa uhodari na Bafilisti. (1 Sa. 9:15-17, 21) “Mangaribi,” ni kusema wakati wafalme wa Israeli hawakukuwa tena natawala, Malkia Esta na Mordekai benye balikuwa bazao ba Benyamini, baliokowa Baisraeli juu basiharibiwe mu utawala wa Uajemi.—Est. 2:5-7; 8:3; 10:3.

18. Namna gani tunaweza kuwa bashikamanifu sawa vile bazao ya Benyamini?

18 Tunajifunza nini? Inawezekana bazao ya Benyamini balifurahi sana kuona mutu wa mu kabila yao anakuwa mufalme. Lakini wakati Yehova aliamua kupatia Daudi wa mu kabila ya Yuda ufalme, bazao ya Benyamini balimutegemeza. (2 Sa. 3:17-19) Kisha miaka mingi, wakati makabila ingine iliasi, balishikamana na Yuda na baliendelea kutegemeza mufalme mwenye Yehova alichagua. (1 Fa. 11:31, 32; 12:19, 21) Leo, na siye tuendelee kutegemeza kwa ushikamanifu benye Yehova amechagua juu ya kutuongoza.—1 Te. 5:12.

19. Mambo yenye Yakobo aliambia batoto yake mbele akufe inatufundisha nini?

19 Mambo yenye Yakobo alitabiri mbele akufe inaweza kutuletea faida. Kuchunguza ile mambo kunatusaidia tuamini kama maunabii yote yenye iko mu Neno ya Mungu itatimia tu. Na kunatusaidia pia kuelewa muzuri mambo yenye tunaweza kufanya juu tumufurahishe Yehova.

WIMBO 128 Vumilia Mupaka Mwisho

a Yakobo alibariki batoto yake ine ba kwanza vile balifuatana kuanzia kwa mukubwa mupaka kwa muloko, ni kusema Rubeni, Simeoni, Lawi, na Yuda. Lakini bale bengine hakubabariki kulingana na namna balifuatana.