MAISHA YA MUKRISTO
Ukuwe Tayari mu hii Sehemu ya Mwisho ya “Siku za Mwisho”
Wakati tuko navumilia hii sehemu ya mwisho ya “siku za mwisho,” tunajua kama magumu itaendelea kuongezeka sana. (2Ti 3:1; Mt 24:8) Wakati wanafikiwa na musiba, mara mingi watu wa Yehova wanapataka maagizo kwa wakati wenye kufaa ili waokoke. Juu tuokoke wakati musiba unafika, inaomba kuanza kujitayarisha sasa, kiroho na kimwili.—Lu 16:10.
-
Kujitayarisha kiroho: Ujizoeze. Ujifunze njia mbalimbali za kuhubiri. Usiogope kama wakati fulani unajikuta uko mbali na ndugu na dada. (Isa 30:15) Yehova na Yesu hawatakuacha.—od uku. 162 fu. 15-17
-
Kujitayarisha kimwili: Zaidi ya kutayarisha sakoshe, kila mutu anapaswa kuwa na chakula fulani ya kutosha, maji, dawa, na mambo ingine yenye inaweza kumusaidia kama inaomba kukimbilia fasi ingine kwa wakati murefu.—Mez 22:3; g17.5 uku. 4, 6
MUANGALIE VIDEO UKO TAYARI KWA AJILI YA MUSIBA WA ASILI? KISHA MUJIBIE HII MAULIZO:
-
Namna gani tunaweza kujitayarisha kiroho kwa ajili ya musiba?
-
Juu ya nini tunapaswa . . .
-
kupatia wazee adresi na namba yetu ya telefone?
-
kutayarisha vitu vya musaada wa kwanza?
-
kuzungumuzia aina ya misiba yenye inaweza kutokea na mambo yenye tunaweza kufanya mu kila hali?
-
-
Ni mambo gani tatu yenye tunaweza kufanya juu ya kusaidia wengine wakati wanafikiwa na musiba?
UJIULIZE HIVI: ‘Hii ugonjwa ya COVID-19, inaweza kunifundisha nini kuhusu kujitayarisha?’