Zaburi 139:1-24
Kwa kiongozi. Ya Daudi. Muziki.
139 Ee Yehova, umenichunguza kabisa, na unanijua.+
2 Unajua wakati ninakaa na wakati ninasimama.+
Unatambua mawazo yangu kwa mbali.+
3 Unanichunguza* wakati ninasafiri na wakati ninalala;Unajua njia zangu zote.+
4 Hakuna neno kwenye ulimi wangu,Lakini angalia! Ee Yehova, tayari unalijua muzuri.+
5 Unanizunguka nyuma na mbele;Na unatia mukono wako juu yangu.
6 Ujuzi wa namna hiyo unapita uelewaji wangu.*
Uko juu sana, siwezi kuufikia.*+
7 Ninaweza kuenda wapi ili kuponyoka roho yako,Na ni wapi ninaweza kukimbia mbali na uso wako?+
8 Kama ningepanda mbinguni, ungekuwa kule,Na kama ningetandika kitanda changu katika Kaburi,* angalia! ungekuwa kule.+
9 Kama ningeruka kwa mabawa ya mapambazuko*Ili niishi pembeni ya bahari ya mbali sana,
10 Hata kule mukono wako ungeniongozaNa mukono wako wa kuume ungenishika.+
11 Kama ninasema: “Hakika giza litanificha!”
Basi usiku wenye kunizunguka ungekuwa mwangaza.
12 Hata giza halingekuwa nzito sana kwako,Lakini usiku ungekuwa wenye kungaa kama muchana;+Kwako giza ni sawa na mwangaza.+
13 Kwa maana uliumba figo zangu;Ulinificha* katika tumbo la uzazi la mama yangu.+
14 Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia yenye kuogopesha sana na ya ajabu.+
Kazi zako ni za ajabu,+Ninajua* muzuri sana jambo hilo.
15 Mifupa yangu haikufichwa mbele ya macho yakoWakati nilifanywa katika siri,Wakati nilisukwa katika sehemu za chini kabisa za dunia.+
16 Macho yako hata yaliniona wakati nilikuwa kiini-tete;Sehemu zake zote ziliandikwa katika kitabu chakoKuhusiana na siku zenye sehemu hizo ziliumbwa,Mbele sehemu yoyote kati ya hizo ikuwe.
17 Kwa hiyo kwangu mimi, mawazo yako ni yenye samani sana!+
Ee Mungu, hesabu yote ya mawazo hayo ni kubwa sana!+
18 Kama ninajaribu kuyahesabu, ni mengi kuliko chembe za muchanga.+
Wakati ninaamuka, ningali pamoja na wewe.*+
19 Ee Mungu, ingekuwa muzuri kama ungeua waovu!+
Halafu watu wenye jeuri* wangeniondokea,
20 Wale wenye kusema mambo ya mubaya juu yako kwa nia yenye uovu;*Wao ni wapinzani wako wenye kutumia jina lako kwa njia yenye haifae.+
21 Je, sichukie wale wenye kukuchukia, Ee Yehova,+Na kuchukia kabisa wale wenye kukuasi?+
22 Ninawachukia kwelikweli;+Wamekuwa maadui wangu kabisa.
23 Unichunguze kabisa, Ee Mungu, na ujue moyo wangu.+
Unichunguze, na ujue mawazo yangu yenye kuhangaisha.*+
24 Angalia kama kuko njia yoyote yenye kuumiza ndani yangu,+Na uniongoze katika njia ya milele.+
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “Unanipima.”
^ Ao “ni wa kushangaza sana kwangu.”
^ Ao “Uko mwingi sana, siwezi kuuelewa.”
^ Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
^ Mapambazuko ni wakati mwangaza wa asubui unaanza kutokea.
^ Ao pengine, “Ulinisuka pamoja.”
^ Ao “Nafsi yangu inajua.”
^ Ao pengine, “nitakuwa ningali ninayahesabu.”
^ Ao “wenye hatia ya damu.”
^ Ao “kulingana na wazo lao.”
^ Ao “yenye kusumbua.”