Zaburi 122:1-9
Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi.
122 Nilishangilia wakati waliniambia:
“Tuende kwenye nyumba ya Yehova.”+
2 Na sasa miguu yetu inasimamaNdani ya milango yako mikubwa, Ee Yerusalemu.+
3 Yerusalemu imejengwa kama mujiWenye kuunganishwa pamoja kama kitu kimoja.+
4 Makabila yamepanda kuenda kwenye muji huo,Makabila ya Yah,*Kulingana na kikumbusho chenye Israeli walipewa,Ili kushukuru jina la Yehova.+
5 Kwa maana viti vya ufalme vya hukumu viliwekwa kule,+Viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.+
6 Muombe Yerusalemu ikuwe na amani.+
Wale wenye kukupenda, Ee muji, watakuwa salama.
7 Amani iendelee ndani ya boma zako,*Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema:
“Amani ikuwe ndani yako.”
9 Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+Nitatafuta mema kwa ajili yako.