Zaburi 122:1-9

  • Sala ya kuomba muji wa Yerusalemu ukuwe na amani

    • Shangwe ya kuenda kwenye nyumba ya Yehova (1)

    • Muji wenye kuunganishwa pamoja kama kitu kimoja (3)

Wimbo wa Safari za Kupanda. Wa Daudi. 122  Nilishangilia wakati waliniambia: “Tuende kwenye nyumba ya Yehova.”+  2  Na sasa miguu yetu inasimamaNdani ya milango yako mikubwa, Ee Yerusalemu.+  3  Yerusalemu imejengwa kama mujiWenye kuunganishwa pamoja kama kitu kimoja.+  4  Makabila yamepanda kuenda kwenye muji huo,Makabila ya Yah,*Kulingana na kikumbusho chenye Israeli walipewa,Ili kushukuru jina la Yehova.+  5  Kwa maana viti vya ufalme vya hukumu viliwekwa kule,+Viti vya ufalme vya nyumba ya Daudi.+  6  Muombe Yerusalemu ikuwe na amani.+ Wale wenye kukupenda, Ee muji, watakuwa salama.  7  Amani iendelee ndani ya boma zako,*Usalama ndani ya minara yako yenye ngome.  8  Kwa ajili ya ndugu zangu na wenzangu nitasema: “Amani ikuwe ndani yako.”  9  Kwa ajili ya nyumba ya Yehova Mungu wetu,+Nitatafuta mema kwa ajili yako.

Maelezo ya Chini

“Yah” ni kifupi cha jina Yehova.
Ao “kuta zako zenye ngome.”