Yona 3:1-10

  • Yona anamutii Mungu na anaenda Ninawi (1-4)

  • Waninawi wanatubu kisha kusikia ujumbe wa Yona (5-9)

  • Mungu anaamua kwamba hataharibu Ninawi (10)

3  Kisha neno la Yehova likakuja kwa Yona mara ya pili, na kusema:+ 2  “Simama, uende Ninawi+ ule muji mukubwa, na utangaze juu yake ujumbe wenye ninakuambia.” 3  Basi Yona akasimama na kuenda Ninawi+ kwa kutii neno la Yehova.+ Sasa Ninawi ulikuwa muji mukubwa sana*—mwendo wa kutembea kwa siku tatu (3). 4  Kisha Yona akaingia katika muji, na kutembea mwendo wa siku moja, alikuwa anatangaza hivi: “Kisha siku makumi ine (40) tu, Ninawi itaharibiwa.” 5  Na watu wa Ninawi wakaanza kumuamini Mungu,+ na wakatangaza kwamba watu wafunge na kuvaa nguo za magunia, kuanzia mukubwa zaidi mupaka mudogo zaidi kati yao. 6  Wakati ujumbe huo ulifikia mufalme wa Ninawi, akasimama kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua nguo yake ya kifalme, akavaa nguo za magunia, na kukaa katika majivu. 7  Zaidi ya hayo, akaamuru tangazo litolewe katika muji wote wa Ninawi,“Mufalme na watu wake wenye vyeo wanatoa amri hii: Hakuna mutu wala munyama, mifugo wala kundi, wenye wanaruhusiwa kula kitu chochote. Hawapaswe kula chakula, wala kunywa maji. 8  Wote wavae nguo za magunia, watu na wanyama; na wamuombe Mungu kwa bidii na kuacha uovu wao na matendo yao ya jeuri. 9  Ni nani anajua kama Mungu wa kweli hatabadilisha nia yake* na kuacha kasirani yake yenye kuwaka, ili tusiangamie?” 10  Wakati Mungu wa kweli aliona mambo yenye walifanya, namna waliacha uovu wao,+ akabadilisha nia yake* kuhusu musiba wenye alisema ataleta juu yao, na hakuuleta.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “muji mukubwa kwa Mungu.”
Ao “hatasikitika.”
Ao “akasikitika.”