Isaya 46:1-13

  • Tofauti kati ya sanamu za Babiloni na Mungu wa Israeli (1-13)

    • Yehova anatabiri mambo ya wakati wenye kuja (10)

    • Ndege mwenye kuwinda kutoka mahali jua linatokea (11)

46  Beli anainama,+ Nebo anajikunja. Sanamu zao zimepakizwa juu ya wanyama, juu ya wanyama wa kubeba mizigo,+Kama mizigo yenye kulemea wanyama wenye kuchoka.  2  Wanajikunja na kuinama pamoja;Hawawezi kuokoa mizigo,*Nao wenyewe wanaenda* katika utekwa.  3  “Munisikilize, Ee nyumba ya Yakobo, na ninyi wote wenye kubakia wa nyumba ya Israeli,+Ninyi wenye nilitegemeza tangu wakati mulizaliwa na kuwabeba tangu tumbo la uzazi.+  4  Mupaka wakati mutazeeka nitakuwa uleule;+Mupaka wakati kichwa chenu kitakuwa na imvi nitaendelea kuwabeba. Kama vile nimefanya, nitawachukua na kuwabeba na kuwaokoa.+  5  Mutanifananisha na nani ao kunifanya kuwa sawa na nani ao kunilinganisha na nani,+Ili tufanane naye?+  6  Kuko wale wenye kutosha zahabu nyingi katika mufuko wao;Wanapima feza kwenye mizani.* Wanalipa fundi wa metali, na anaitengeneza kuwa mungu.+ Kisha wanainamisha uso mupaka chini, ndiyo, wanaiabudu.*+  7  Wanainyangula na kuitia kwenye mabega yao;+Wanaibeba na kuitia mahali pake, na inasimama tu pale. Haiondoke mahali pake.+ Wanasema nayo kwa sauti kubwa, lakini haijibu;Haiwezi kuokoa mutu yeyote katika taabu.+  8  Mukumbuke jambo hili, na mujipe moyo. Muliweke katika moyo, ninyi wakosaji.  9  Mukumbuke mambo ya kwanza ya zamani sana,Kwamba mimi ni Mungu na hakuna mwingine. Mimi ni Mungu na hakuna mwenye kuwa kama mimi.+ 10  Ninatabiri matokeo tangu mwanzoNa tangu zamani sana mambo yenye bado hayajafanywa.+ Ninasema, ‘Uamuzi wangu utasimama,*+Na nitafanya jambo lolote lenye ninapenda.’+ 11  Ninaita ndege mwenye kuwinda kutoka mahali jua linatokea,*+Kutoka inchi ya mbali mutu mwenye atatimiza uamuzi wangu.*+ Nimesema, na nitafanya litokee. Nimekusudia, na pia nitalitimiza.+ 12  Munisikilize, ninyi wenye moyo mugumu,*Ninyi wenye kuwa mbali na haki. 13  Nimeleta karibu haki yangu;Haiko mbali,Na wokovu wangu hautachelewa.+ Nitaleta wokovu katika Sayuni, na utukufu wangu kwa Israeli.”+

Maelezo ya Chini

Ni kusema, sanamu zenye kupakizwa juu ya wanyama.
Ao “Na nafsi zao zinaenda.”
Ao “kilo.”
Tnn., “wanaiinamia.”
Ao “Kusudi langu litasimama; Shauri langu litasimama.”
Ao “mashariki.”
Ao “kusudi langu; shauri langu.”
Tnn., “moyo wenye nguvu.”