Ezekieli 2:1-10

  • Ezekieli anapewa mugao wa kuwa nabii (1-10)

    • ‘Kama watasikiliza ao hapana’ (5)

    • Anaonyeshwa kitabu cha kukunjwa chenye nyimbo za huzuni (9, 10)

2  Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu,* simama kwa miguu yako ili nizungumuze na wewe.”+ 2  Wakati alizungumuza na mimi, roho ikaingia ndani yangu na kunifanya nisimame kwa miguu yangu+ ili niweze kumusikia Ule mwenye kuzungumuza na mimi. 3  Akaendelea kuniambia: “Mwana wa binadamu, ninakutuma kwa watu wa Israeli,+ kwa mataifa yenye kuasi ambayo yameniasi.+ Wao na mababu zao wamenikosea mupaka leo hii.+ 4  Ninakutuma kwa wana wenye kuwa kichwa-nguvu* na wenye moyo mugumu,+ na unapaswa kuwaambia, ‘Haya ndiyo mambo yenye Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.’ 5  Nao, kama watasikiliza ao watakataa kusikiliza​—⁠kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi+​—⁠hakika watajua pia kwamba nabii alikuwa kati yao.+ 6  “Lakini wewe, mwana wa binadamu, usiwaogope,+ na usiogope maneno yao, hata kama umezungukwa na michongoma na miiba*+ na unakaa kati ya nge. Usiogope maneno yao+ na usitishwe na nyuso zao,+ kwa maana wao ni nyumba yenye kuasi. 7  Unapaswa kuwaambia maneno yangu, kama watasikiliza ao hapana, kwa maana wao ni watu wenye kuasi.+ 8  “Lakini wewe, mwana wa binadamu, sikiliza kile ninakuambia. Usikuwe muasi kama nyumba hii yenye kuasi. Fungua kinywa chako na ukule kile ninakupatia.”+ 9  Wakati niliangalia, niliona mukono wenye ulikuwa umenyooshwa kunielekea,+ na katika mukono huo niliona kitabu cha kukunjwa chenye kuandikwa.+ 10  Wakati alikikunjua mbele yangu, kilikuwa kimeandikwa mbele na nyuma.+ Nyimbo za huzuni* na maombolezo na vilio vilikuwa vimeandikwa kwenye kitabu hicho.+

Maelezo ya Chini

“Mwana wa binadamu”; hii ni mara ya kwanza kati ya mara 93 yenye maneno haya yanapatikana katika kitabu cha Ezekieli.
Ao “wenye uso mugumu.”
Ao pengine, “hata kama watu wako kichwa-nguvu na wako kama vitu vyenye kukutoboa-toboa.”
Ao “Nyimbo za maombolezo.”