Cha Kwanza cha Mambo ya Nyakati 16:1-43
16 Basi wakaingiza Sanduku la Mungu wa kweli na kuliweka ndani ya hema yenye Daudi alikuwa ameisimamishia;+ na wakatoa matoleo ya kuteketezwa na zabihu za ushirika mbele ya Mungu wa kweli.+
2 Wakati Daudi alimaliza kutoa matoleo ya kuteketezwa+ na zabihu za ushirika,+ akabariki watu katika jina la Yehova.
3 Tena, aligawia Waisraeli wote, kila mwanaume na mwanamuke, mukate mumoja wa muviringo, keki ya tende, na keki ya zabibu zenye kukauka.
4 Kisha akaweka Walawi fulani wafanye utumishi mbele ya Sanduku la Yehova,+ wamuheshimie,* wamushukuru, na wamusifu Yehova Mungu wa Israeli.
5 Asafu+ alikuwa kichwa, na wa pili kisha yeye alikuwa Zekaria; na Yeieli, Shemiramoti, Yehieli, Matitia, Eliabu, Benaya, Obed-edomu, na Yeieli+ walipiga vyombo vya kamba na vinubi;+ na Asafu alipiga matoazi,+
6 na Benaya na Yahazieli makuhani walipiga tarumbeta bila kuacha mbele ya sanduku la agano la Mungu wa kweli.
7 Hiyo ndiyo siku yenye Daudi kwa mara ya kwanza alitoa muchango wa wimbo wenye alitunga ili kumushukuru Yehova na akaupatia Asafu+ na ndugu zake:
8 “Mumushukuru Yehova,+ muitie jina lake,Mujulishe matendo yake kati ya vikundi vya watu!+
9 Mumuimbie, mumuimbie sifa,*+Mufikiri sana* juu ya kazi zake zote za ajabu.+
10 Mujisifu juu ya jina lake takatifu.+
Mioyo ya wale wenye kumutafuta Yehova ishangilie.+
11 Mumutafute Yehova+ na nguvu zake,Mutafute uso wake* bila kuacha.+
12 Mukumbuke kazi za ajabu zenye amefanya,+Miujiza yake na hukumu zenye ametangaza,
13 Ninyi uzao wa* Israeli mutumishi wake,+Ninyi wana wa Yakobo, wachaguliwa wake.+
14 Yeye ni Yehova Mungu wetu.+
Hukumu zake ziko katika dunia yote.+
15 Mukumbuke agano lake milele,Ahadi yenye alitoa,* mupaka vizazi elfu,+
16 Agano lenye alifanya pamoja na Abrahamu,+Na kiapo chenye alimuapia Isaka,+
17 Chenye aliweka kuwa amri kwa Yakobo+Na kuwa agano la kudumu kwa Israeli,
18 Akisema, ‘Nitakupatia inchi ya Kanaani+Kuwa uriti wenu wenye muligawiwa.’+
19 Ilikuwa vile wakati mulikuwa watu kidogo,Ndiyo, kidogo sana, na mulikuwa wageni katika inchi.+
20 Walitembea-tembea kutoka taifa moja mupaka taifa lingine,Kutoka ufalme mumoja mupaka kikundi kingine cha watu.+
21 Hakumuruhusu mutu yeyote awakandamize,+Lakini kwa sababu yao alikaripia wafalme,+
22 Akisema, ‘Musiguse watiwa-mafuta wangu,Na musitendee manabii wangu jambo lolote la mubaya.’+
23 Mumuimbie Yehova, dunia yote!
Mutangaze wokovu wake siku kwa siku!+
24 Mutangaze utukufu wake kati ya mataifa,Kazi zake za ajabu kati ya vikundi vyote vya watu.
25 Kwa maana Yehova ni mukubwa na anastahili kusifiwa sana.
Ni mwenye kuogopesha sana kuliko miungu mingine yote.+
26 Miungu yote ya vikundi vya watu ni miungu yenye haina mafaa yoyote,+Lakini Yehova ndiye alifanya mbingu.+
27 Mbele yake kuko ukubwa* na utukufu;+Nguvu na furaha viko katika makao yake.+
28 Mumupatie Yehova kile chenye anastahili, ninyi familia za vikundi vya watu,Mumupatie Yehova kile chenye anastahili kwa sababu ya utukufu wake na nguvu zake.+
29 Mumupatie Yehova utukufu wenye jina lake linastahili;+Mulete zawadi na muingie mbele yake.+
Mumuinamie* Yehova katika mapambo matakatifu.*+
30 Mutetemeke mbele yake, dunia yote!
Dunia* imewekwa imara kabisa; haiwezi kuhamishwa.*+
31 Mbingu zishangilie, na dunia ifurahi;+Mutangaze kati ya mataifa: ‘Yehova amekuwa Mufalme!’+
32 Bahari ingurume na vyote vyenye kuijaza;Maeneo ya mashamba na vyote vyenye kuwa ndani yake vishangilie.
33 Wakati uleule miti ya pori ipige vigelegele vya shangwe mbele ya Yehova,Kwa maana anakuja* kuhukumu dunia.
34 Mumushukuru Yehova, kwa maana yeye ni mwema;+Upendo wake mushikamanifu unadumu milele.+
35 Na museme, ‘Utuokoe, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Utukusanye na kutuokoa kutoka kwa mataifa,Ili tushukuru jina lako takatifu+Na tukusifu kwa shangwe.*+
36 Yehova Mungu wa Israeli, asifiweKwa umilele wote.’”*
Na watu wote wakasema, “Amina!”* na wakamusifu Yehova.
37 Kisha Daudi akaacha Asafu+ na ndugu zake pale mbele ya sanduku la agano la Yehova ili wafanye utumishi bila kuacha mbele ya Sanduku hilo,+ kulingana na kawaida ya kila siku.+
38 Obed-edomu na ndugu zake, watu makumi sita na munane (68), na Obed-edomu mwana wa Yedutuni, na Hosa walikuwa walinzi wa milango mikubwa;
39 na Sadoki+ kuhani na makuhani wenzake walikuwa mbele ya tabenakulo ya Yehova mahali pa juu kule Gibeoni+
40 ili kumutolea Yehova kwa ukawaida matoleo ya kuteketezwa kwenye mazabahu ya toleo la kuteketezwa, asubui na mangaribi, na kufanya mambo yote yenye yameandikwa katika Sheria ya Yehova yenye aliamuru Israeli.+
41 Pamoja nao kulikuwa Hemani na Yedutuni+ na wanaume wengine wenye walichaguliwa wenye walitajwa kwa majina yao ili wamushukuru Yehova,+ kwa sababu “upendo wake mushikamanifu unadumu milele”;+
42 na pamoja nao kulikuwa Hemani+ na Yedutuni ili wapige tarumbeta, matoazi, na vyombo vyenye vilitumiwa ili kumusifu* Mungu wa kweli; na wana wa Yedutuni+ walikuwa kwenye mulango mukubwa.
43 Kisha watu wote wakaenda kwao, na Daudi akaenda kubariki nyumba yake mwenyewe.
Maelezo ya Chini
^ Tnn., “wamukumbuke.”
^ Ao “mumupigie muziki.”
^ Ao pengine, “Museme.”
^ Ao “kuwapo kwake.”
^ Ao “wazao wa.” Tnn., “mbegu ya.”
^ Tnn., “Neno lenye aliamuru.”
^ Ao “heshima.”
^ Ao “Mumuabudu.”
^ Ao pengine, “kwa sababu ya utukufu wa utakatifu wake.”
^ Ao “Inchi yenye kuzaa.”
^ Ao “kutikiswa.”
^ Ao “amekuja.”
^ Ao “tushangilie katika sifa yako.”
^ Ao “Tangu milele mupaka milele.”
^ Ao “Ikuwe vile!”
^ Ao “vyombo vya wimbo wa.”