YESU​—NJIA, KWELI, NA UZIMA

Huduma ya Mwisho ya Yesu

Kiswahili
Huduma ya Mwisho ya Yesu
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1102014746/univ/art/1102014746_univ_sqr_xl.jpg
jy kur. 234-235

SEHEMU YA 6

Huduma ya Mwisho ya Yesu

“Mfalme Wako Anakuja Kwako.”​—Mathayo 21:5

Huduma ya Mwisho ya Yesu

KATIKA SEHEMU HII

SURA YA 101

Mlo Katika Nyumba ya Simoni Huko Bethania

Maria, dada yake Lazaro, anafanya jambo linalotokeza mabishano, lakini Yesu anamtetea.

SURA YA 102

Mfalme Aingia Yerusalemu Akiwa Juu ya Mwanapunda

Anatimiza unabii uliotolewa miaka mia tano mapema.

SURA YA 103

Hekalu Lasafishwa Tena

Wafanyabiashara walio Yerusalemu wanaonekana kuwa wanafanya biashara halali, basi kwa nini Yesu anawaita wanyang’anyi?

SURA YA 104

Wayahudi Wasikia Sauti ya Mungu​—Je, Wataonyesha Imani?

Je, kuna tofauti kati ya kumwamini Yesu na kutenda kulingana na imani hiyo?

SURA YA 105

Atumia Mtini Kufundisha Kuhusu Imani

Yesu awafundisha wanafunzi wake kuhusu nguvu za imani na kueleza sababu inayofanya Mungu alikatae taifa la Israeli.

SURA YA 106

Mifano Miwili Kuhusu Mashamba ya Mizabibu

Soma kuhusu maana ya mfano wa mtu aliyewaomba wanawe wakafanye kazi katika shamba lake la mizabibu na mfano wa mtu aliyewakodisha wakulima waovu shamba lake la mizabibu.

SURA YA 107

Mfalme Awaita Wale Walioalikwa Kwenye Karamu ya Ndoa

Kwa kweli mfano wa Yesu ni unabii.

SURA YA 108

Yesu Apangua Njama za Kumtega

Kwanza anawanyamazisha Mafarisayo, kisha Masadukayo, na mwishowe muungano wa wapinzani wake.

SURA YA 109

Awashutumu Wapinzani wa Kidini

Kwa nini Yesu havumilii tofauti za kidini?

SURA YA 110

Siku ya Mwisho ya Yesu Hekaluni

Anatumia mfano wa mjane maskini kufundisha somo muhimu sana.

SURA YA 111

Mitume Waomba Ishara

Unabii wake ulikuwa na utimizo wa kwanza katika karne ya kwanza. Je, utakuwa na utimizo mkubwa wakati ujao?

SURA YA 112

Somo Kuhusu Kuwa Macho​—Mabikira

Je, Yesu alifundisha kwamba nusu ya wanafunzi wake ni wapumbavu na nusu nyingine ni wenye busara?

SURA YA 113

Somo Kuhusu Bidii​—Talanta

Mfano wa Yesu unafafanua maneno yake: “Kila mtu aliye na kitu ataongezewa.”

SURA YA 114

Kristo Akiwa na Mamlaka Awahukumu Kondoo na Mbuzi

Yesu anatumia mfano unaoeleweka kufafanua msingi wa hukumu ya milele.

SURA YA 115

Pasaka ya Mwisho ya Yesu Yakaribia

Kwa nini viongozi wa kidini wanakubali kumlipa Yuda vipande 30 tu vya fedha ili kumsaliti Yesu?

SURA YA 116

Afundisha Kuhusu Unyenyekevu Kwenye Pasaka ya Mwisho

Anawashangaza mitume kwa kufanya kazi ya mtumwa.

SURA YA 117

Mlo wa Jioni wa Bwana

Yesu anaanzisha mwadhimisho ambao wanafunzi wake wanapaswa kufanya siku ya Nisani 14 kila mwaka.

SURA YA 118

Wabishana Kuhusu Aliye Mkuu Zaidi

Tayari mitume wamesahau somo ambalo Yesu aliwafundisha mapema jioni ya siku hiyo.

SURA YA 119

Yesu​—Njia, Kweli, na Uzima

Yesu anafundisha ukweli muhimu kuhusu jinsi ya kufika kwa Mungu.

SURA YA 120

Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Rafiki za Yesu

Wanafunzi wa Yesu ‘wanazaa matunda’ kwa njia gani?

SURA YA 121

“Jipeni Moyo! Mimi Nimeushinda Ulimwengu”

Yesu aliushindaje ulimwengu ingawa ulimwengu ulimuua?

SURA YA 122

Sala ya Mwisho ya Yesu Katika Chumba cha Juu

Anataja wazi kwamba alitimiza jambo muhimu kuliko kuwaletea wanadamu wokovu.

SURA YA 123

Yesu Anasali Akiwa na Huzuni Nyingi

Kwa nini Yesu anasali hivi: “Niondolee kikombe hiki”? Je, anakimbia jukumu lake la kufa ili kutoa fidia?

SURA YA 124

Kristo Asalitiwa na Kukamatwa

Yuda anafaulu kumpata Yesu ingawa ni usiku wa manane.

SURA YA 125

Yesu Apelekwa kwa Anasi, Kisha kwa Kayafa

Kesi ya Yesu haifanywi kwa haki.

SURA YA 126

Akanwa Nyumbani kwa Kayafa

Petro mwanamume mwenye imani na ujitoaji angewezaje kumgeuka Yesu haraka sana hivyo?

SURA YA 127

Kesi Mbele ya Sanhedrini, Kisha Apelekwa kwa Pilato

Viongozi wa kidini wa Wayahudi wanafunua kusudi lao halisi.

SURA YA 128

Pilato na Herode Wakosa Kumpata Yesu na Hatia

Kwa nini Pilato anaagiza Yesu akahukumiwe na Herode? Je, Pilato hana mamlaka ya kumhukumu Yesu?

SURA YA 129

Pilato Asema: “Tazama! Mwanamume!”

Hata Pilato anatambua sifa nzuri ambazo Yesu anaonyesha.

SURA YA 130

Yesu Akabidhiwa na Kupelekwa Akauawe

Kwa nini Yesu anawaambia wanawake wanaomboleza walie kwa ajili yao wenyewe na watoto wao badala ya kumlilia Yesu?

SURA YA 131

Mfalme Asiye na Hatia Ateseka Kwenye Mti

Yesu anampa ahadi kubwa mmoja wa wahalifu wanaoteswa pamoja naye.

SURA YA 132

“Hakika Mtu Huyu Alikuwa Mwana wa Mungu”

Giza linalotokea kimuujiza, tetemeko kali, na kupasuka kwa pazia la hekaluni kunathibitisha jambo moja.

SURA YA 133

Mwili wa Yesu Watayarishwa na Kuzikwa

Kwa nini mwili wa Yesu unazikwa haraka haraka kabla ya jua kutua?

SURA YA 134

Kaburi Tupu​—Yesu Yuko Hai!

Baada ya kufufuliwa, Yesu anajionyesha kwanza kwa mwanafunzi mwanamke badala ya mitume wake.

SURA YA 135

Yesu Aliyefufuliwa Awatokea Wengi

Yesu anawathibitishiaje wanafunzi wake kwamba amefufuliwa?

SURA YA 136

Kwenye Ufuo wa Bahari ya Galilaya

Petro anakumbushwa mara tatu jinsi anavyoweza kuonyesha kwamba anampenda Yesu.

SURA YA 137

Mamia Wamwona Kabla ya Pentekoste

Baada ya kufufuliwa na kabla ya kwenda mbinguni, Yesu anawasisitizia tena na tena wanafunzi wake kile watakachopokea na jinsi wanavyopaswa kukitumia.

SURA YA 138

Kristo Akiwa Kwenye Mkono wa Kuume wa Mungu

Yesu angekuwa akifanya nini alipokuwa akisubiri wakati wa kuwachukulia hatua maadui wake ufike?

SURA YA 139

Yesu Aleta Paradiso na Kumaliza Mgawo Wake

Bado ana mengi ya kufanya kabla ya kumkabidhi Ufalme Mungu na Baba yake.