SEHEMU YA 6
Huduma ya Mwisho ya Yesu
“Mfalme Wako Anakuja Kwako.”—Mathayo 21:5
KATIKA SEHEMU HII
SURA YA 101
Mlo Katika Nyumba ya Simoni Huko Bethania
Maria, dada yake Lazaro, anafanya jambo linalotokeza mabishano, lakini Yesu anamtetea.
SURA YA 102
Mfalme Aingia Yerusalemu Akiwa Juu ya Mwanapunda
Anatimiza unabii uliotolewa miaka mia tano mapema.
SURA YA 103
Hekalu Lasafishwa Tena
Wafanyabiashara walio Yerusalemu wanaonekana kuwa wanafanya biashara halali, basi kwa nini Yesu anawaita wanyang’anyi?
SURA YA 104
Wayahudi Wasikia Sauti ya Mungu—Je, Wataonyesha Imani?
Je, kuna tofauti kati ya kumwamini Yesu na kutenda kulingana na imani hiyo?
SURA YA 105
Atumia Mtini Kufundisha Kuhusu Imani
Yesu awafundisha wanafunzi wake kuhusu nguvu za imani na kueleza sababu inayofanya Mungu alikatae taifa la Israeli.
SURA YA 106
Mifano Miwili Kuhusu Mashamba ya Mizabibu
Soma kuhusu maana ya mfano wa mtu aliyewaomba wanawe wakafanye kazi katika shamba lake la mizabibu na mfano wa mtu aliyewakodisha wakulima waovu shamba lake la mizabibu.
SURA YA 108
Yesu Apangua Njama za Kumtega
Kwanza anawanyamazisha Mafarisayo, kisha Masadukayo, na mwishowe muungano wa wapinzani wake.
SURA YA 110
Siku ya Mwisho ya Yesu Hekaluni
Anatumia mfano wa mjane maskini kufundisha somo muhimu sana.
SURA YA 111
Mitume Waomba Ishara
Unabii wake ulikuwa na utimizo wa kwanza katika karne ya kwanza. Je, utakuwa na utimizo mkubwa wakati ujao?
SURA YA 112
Somo Kuhusu Kuwa Macho—Mabikira
Je, Yesu alifundisha kwamba nusu ya wanafunzi wake ni wapumbavu na nusu nyingine ni wenye busara?
SURA YA 113
Somo Kuhusu Bidii—Talanta
Mfano wa Yesu unafafanua maneno yake: “Kila mtu aliye na kitu ataongezewa.”
SURA YA 114
Kristo Akiwa na Mamlaka Awahukumu Kondoo na Mbuzi
Yesu anatumia mfano unaoeleweka kufafanua msingi wa hukumu ya milele.
SURA YA 115
Pasaka ya Mwisho ya Yesu Yakaribia
Kwa nini viongozi wa kidini wanakubali kumlipa Yuda vipande 30 tu vya fedha ili kumsaliti Yesu?
SURA YA 116
Afundisha Kuhusu Unyenyekevu Kwenye Pasaka ya Mwisho
Anawashangaza mitume kwa kufanya kazi ya mtumwa.
SURA YA 117
Mlo wa Jioni wa Bwana
Yesu anaanzisha mwadhimisho ambao wanafunzi wake wanapaswa kufanya siku ya Nisani 14 kila mwaka.
SURA YA 118
Wabishana Kuhusu Aliye Mkuu Zaidi
Tayari mitume wamesahau somo ambalo Yesu aliwafundisha mapema jioni ya siku hiyo.
SURA YA 119
Yesu—Njia, Kweli, na Uzima
Yesu anafundisha ukweli muhimu kuhusu jinsi ya kufika kwa Mungu.
SURA YA 120
Kuzaa Matunda Kama Matawi na Kuwa Rafiki za Yesu
Wanafunzi wa Yesu ‘wanazaa matunda’ kwa njia gani?
SURA YA 121
“Jipeni Moyo! Mimi Nimeushinda Ulimwengu”
Yesu aliushindaje ulimwengu ingawa ulimwengu ulimuua?
SURA YA 122
Sala ya Mwisho ya Yesu Katika Chumba cha Juu
Anataja wazi kwamba alitimiza jambo muhimu kuliko kuwaletea wanadamu wokovu.
SURA YA 123
Yesu Anasali Akiwa na Huzuni Nyingi
Kwa nini Yesu anasali hivi: “Niondolee kikombe hiki”? Je, anakimbia jukumu lake la kufa ili kutoa fidia?
SURA YA 126
Akanwa Nyumbani kwa Kayafa
Petro mwanamume mwenye imani na ujitoaji angewezaje kumgeuka Yesu haraka sana hivyo?
SURA YA 127
Kesi Mbele ya Sanhedrini, Kisha Apelekwa kwa Pilato
Viongozi wa kidini wa Wayahudi wanafunua kusudi lao halisi.
SURA YA 128
Pilato na Herode Wakosa Kumpata Yesu na Hatia
Kwa nini Pilato anaagiza Yesu akahukumiwe na Herode? Je, Pilato hana mamlaka ya kumhukumu Yesu?
SURA YA 129
Pilato Asema: “Tazama! Mwanamume!”
Hata Pilato anatambua sifa nzuri ambazo Yesu anaonyesha.
SURA YA 130
Yesu Akabidhiwa na Kupelekwa Akauawe
Kwa nini Yesu anawaambia wanawake wanaomboleza walie kwa ajili yao wenyewe na watoto wao badala ya kumlilia Yesu?
SURA YA 131
Mfalme Asiye na Hatia Ateseka Kwenye Mti
Yesu anampa ahadi kubwa mmoja wa wahalifu wanaoteswa pamoja naye.
SURA YA 132
“Hakika Mtu Huyu Alikuwa Mwana wa Mungu”
Giza linalotokea kimuujiza, tetemeko kali, na kupasuka kwa pazia la hekaluni kunathibitisha jambo moja.
SURA YA 133
Mwili wa Yesu Watayarishwa na Kuzikwa
Kwa nini mwili wa Yesu unazikwa haraka haraka kabla ya jua kutua?
SURA YA 134
Kaburi Tupu—Yesu Yuko Hai!
Baada ya kufufuliwa, Yesu anajionyesha kwanza kwa mwanafunzi mwanamke badala ya mitume wake.
SURA YA 135
Yesu Aliyefufuliwa Awatokea Wengi
Yesu anawathibitishiaje wanafunzi wake kwamba amefufuliwa?
SURA YA 136
Kwenye Ufuo wa Bahari ya Galilaya
Petro anakumbushwa mara tatu jinsi anavyoweza kuonyesha kwamba anampenda Yesu.
SURA YA 137
Mamia Wamwona Kabla ya Pentekoste
Baada ya kufufuliwa na kabla ya kwenda mbinguni, Yesu anawasisitizia tena na tena wanafunzi wake kile watakachopokea na jinsi wanavyopaswa kukitumia.
SURA YA 138
Kristo Akiwa Kwenye Mkono wa Kuume wa Mungu
Yesu angekuwa akifanya nini alipokuwa akisubiri wakati wa kuwachukulia hatua maadui wake ufike?
SURA YA 139
Yesu Aleta Paradiso na Kumaliza Mgawo Wake
Bado ana mengi ya kufanya kabla ya kumkabidhi Ufalme Mungu na Baba yake.

