Privacy Settings

To provide you with the best possible experience, we use cookies and similar technologies. Some cookies are necessary to make our website work and cannot be refused. You can accept or decline the use of additional cookies, which we use only to improve your experience. None of this data will ever be sold or used for marketing. To learn more, read the Global Policy on Use of Cookies and Similar Technologies. You can customize your settings at any time by going to Privacy Settings.

Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Biblia iliyofunguliwa

HABARI KUU

Je, Biblia Ina Faida Leo?

Je, Biblia Ina Faida Leo?

‘Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nilipata furaha.’

HILTON alipenda mchezo wa ndondi. Akiwa na umri wa miaka saba alikuwa akipigana na watu si tu kwenye jukwaa la ndondi bali pia mitaani. Alipojiunga na shule ya upili (sekondari) yeye na rafiki zake walizurura wakitafuta mtu wa kumpiga. Anasimulia hivi: “Nilikuwa mwizi, nilicheza kamari, niliwanyanyasa wanawake, nilitazama ponografia, na kuwatukana wazazi wangu. Tabia yangu iliharibika hivi kwamba wazazi wangu walifikiri nisingeweza kubadilika. Baada ya kumaliza shule ya upili, niliondoka nyumbani.”

Aliporudi nyumbani baada ya miaka 12, wazazi wake hawakuamini macho yao! Hilton alikuwa mtulivu, mpole, na mwenye heshima. Ni nini kilichomfanya abadilike? Alipokuwa mbali na nyumbani, alitafakari sana kuhusu maisha yake. Pia, alianza kuichunguza Biblia ili imsaidie kubadilisha mwenendo wake. Anasema hivi: “Nilitumia mambo niliyojifunza katika Biblia. Mambo hayo yalitia ndani kuuvua utu wangu wa zamani na kutii amri inayopatikana kwenye andiko la Waefeso 6:2, 3 linalosema kwamba ninapaswa kuwatii wazazi wangu. Kwa mara ya kwanza maishani mwangu, nilipata furaha ya kweli na kuwafurahisha wazazi wangu.”

Simulizi la Hilton linaonyesha jinsi Biblia ilivyo na nguvu ya kumbadili mtu na jinsi viwango vyake vilivyo na faida. (Waebrania 4:12) Acheni tuchunguze baadhi ya viwango hivyo, kama vile: unyoofu, kujizuia, uaminifu, na upendo—na tuone jinsi vinavyoweza kuboresha maisha yetu.