Nidhamu—Uthibitisho wa Upendo wa Yehova
Nidhamu humaanisha kupigwa, kurekebishwa, kuagizwa, na kuelimishwa. Kama baba mwenye upendo anavyowatia nidhamu watoto wake, Yehova hututia nidhamu. Tunatiwa nidhamu kupitia . . .
-
Usomaji wa Biblia, funzo la kibinafsi, kuhudhuria mikutano, na kutafakari
-
Shauri au rekebisho kutoka kwa mwamini mwenzetu
-
Matokeo ya makosa yetu
-
Kukaripiwa kihukumu au kutengwa
-
Majaribu au mateso ambayo Yehova anaruhusu.—w15 9/15 21 ¶13; it-1 629