MAISHA YA MKRISTO
Unaweza Kujifunza Nini Kutoka Kwao?
Je, umewekwa rasmi hivi karibuni kuwa mtumishi wa huduma au mzee? Unaweza kuwa na ujuzi, uwezo, au elimu ambayo wazee au watumishi wa huduma wengine hawana. Hata hivyo, kuna mambo mengi unayoweza kujifunza kutoka kwa akina ndugu hao na kutoka kwa wanaume wa kiroho ambao kwa sasa hawatumikii katika mapendeleo hayo kwa sababu ya umri, matatizo ya afya, au majukumu ya familia.
TAZAMENI VIDEO WAHESHIMU NDUGU WENYE UZOEFU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
-
1. Ndugu Richards alionyeshaje kwamba alimheshimu Ndugu Bello?
-
2. Ben alifanya kosa gani, na kwa nini?
-
3. Ben alijifunza somo gani kutokana na mfano wa Elisha?
-
4. Iwe wewe ni ndugu au dada, unaweza kuonyeshaje kwamba unawaheshimu Wakristo wengine wenye uzoefu na kujifunza kutoka kwao?