Privacy Settings

To provide you with the best possible experience, we use cookies and similar technologies. Some cookies are necessary to make our website work and cannot be refused. You can accept or decline the use of additional cookies, which we use only to improve your experience. None of this data will ever be sold or used for marketing. To learn more, read the Global Policy on Use of Cookies and Similar Technologies. You can customize your settings at any time by going to Privacy Settings.

Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

HAZINA ZA NENO LA MUNGU

Yehova Anawapanga Watu Wake

Yehova Anawapanga Watu Wake

[Onyesha video yenye kichwa Utangulizi wa Hesabu.]

Waisraeli walipiga kambi kulingana na makundi ya makabila matatu (Hes 1:52, 53; w94 12/1 9 ¶4)

Huenda kambi yote ya Waisraeli ilikuwa na jumla ya watu 3,000,000 au zaidi (Hes 2:32, 33; it-1 397 ¶4)

Yehova anataka watu wake wamwabudu kwa mpango. Taifa la Israeli lilimwabudu hivyo, nasi tunamwabudu vivyo hivyo leo.—1Ko 14:33, 40.

Mwonekano wa mpangilio wa kambi ya Waisraeli. Hema la ibada liko katikati. Karibu na hema la ibada kulikuwa na familia za kabila la Walawi: Haruni upande wa mashariki, Wakohathi upande wa kusini, Wagershoni upande wa magharibi, na Wamerari upande wa kaskazini. Makabila 12 ya Waisraeli yako mbali zaidi. Upande wa mashariki kuna kabila la Isakari, Yuda, na Zabuloni. Upande wa kusini kuna kabila la Gadi, Rubeni na Simeoni. Upande wa magharibi kuna kabila la Benjamini, Efraimu, na Manase. Upande wa kaskazini kuna kabila la Naftali, Dani, na Asheri.

JIULIZE, ‘Ninaweza kuonyeshaje kwamba ninaunga mkono tengenezo la Yehova kikamili?’