BIBLIA TAKATIFU—TAFSIRI YA ULIMWENGU MPYA (TOLEO LA 2017)

Utangulizi wa Neno la Mungu

Kiswahili
Utangulizi wa Neno la Mungu
https://cms-imgp.jw-cdn.org/img/p/1001061100/univ/wpub/1001061100_univ_sqr_xl.jpg
nwt uku. 5

Utangulizi wa Neno la Mungu

Biblia ina ujumbe wa Mungu kwa ajili yetu leo. Inatuonyesha jinsi ya kuishi kwa mafanikio na jinsi ya kupata kibali cha Mungu. Pia, inajibu maswali yafuatayo:

JINSI YA KUPATA MISTARI YA BIBLIA

Biblia ina vitabu vidogo 66. Imegawanywa katika sehemu mbili: Maandiko ya Kiebrania na Kiaramu (“Agano la Kale”) na Maandiko ya Kigiriki (“Agano Jipya”). Kila kitabu cha Biblia kimegawanywa kwa sura na mistari. Maandiko yanapotajwa, nambari ya kwanza baada ya jina la kitabu inaonyesha sura, na nambari inayofuata au zinazofuata ni mstari au mistari. Kwa mfano, Mwanzo 1:1 inamaanisha Mwanzo sura ya 1, mstari wa 1.