Zaburi 138:1-8
Ya Daudi.
138 Nitakusifu kwa moyo wangu wote.+Mbele ya miungu mingine nitakupigia muziki.+
2 Nitainama kuelekea hekalu lako takatifu,+Nami nitalisifu jina lako,+Kwa sababu ya fadhili zako zenye upendo+ na kwa sababu ya ukweli wako.+Kwa maana umeyatukuza maneno yako+ hata juu ya jina lako lote.+
3 Katika siku niliyoita, ulinijibu;+Ukaanza kunifanya niwe jasiri katika nafsi yangu kwa nguvu.+
4 Wafalme wote wa dunia watakusifu wewe, Ee Yehova,+Kwa maana watakuwa wameyasikia maneno ya kinywa chako.
5 Nao wataimba juu ya njia za Yehova,+Kwa maana utukufu wa Yehova ni mkuu.+
6 Kwa maana Yehova yuko juu, hata hivyo yeye humwona mnyenyekevu;+Lakini yeye anamjua mwenye kiburi kutoka mbali tu.+
7 Kama nikitembea katikati ya taabu, wewe utanihifadhi hai.+Kwa sababu ya hasira ya adui zangu wewe utaunyoosha mkono,+Na mkono wako wa kuume utaniokoa.+
8 Yehova mwenyewe atayamalizia mambo yaliyoko kwa ajili yangu.+Ee Yehova, fadhili zako zenye upendo ni za mpaka wakati usio na kipimo.+Usiziache kazi za mikono yako mwenyewe.+