Zaburi 113:1-9

113  Msifuni Yah!+Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+Lisifuni jina la Yehova.+   Jina la Yehova na libarikiwe+Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+   Kutoka mapambazuko ya jua mpaka kutua kwake+Jina la Yehova ni la kusifiwa.+   Yehova amekuwa juu ya mataifa yote;+Utukufu wake uko juu ya mbingu.+   Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+Yeye anayefanya makao yake juu?+   Yeye anajishusha kutazama mbingu na dunia,+   Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi;+Humwinua maskini kutoka kwenye shimo la majivu,+   Ili kumketisha pamoja na wenye vyeo,+Wenye vyeo kati ya watu wake.+   Anampa mwanamke tasa makao katika nyumba+Kama mama ya wana aliye na shangwe.+Msifuni Yah!+

Maelezo ya Chini