Zaburi 113:1-9
113 Msifuni Yah!+Toeni sifa, enyi watumishi wa Yehova,+Lisifuni jina la Yehova.+
2 Jina la Yehova na libarikiwe+Kutoka sasa mpaka wakati usio na kipimo.+
3 Kutoka mapambazuko ya jua mpaka kutua kwake+Jina la Yehova ni la kusifiwa.+
4 Yehova amekuwa juu ya mataifa yote;+Utukufu wake uko juu ya mbingu.+
5 Ni nani aliye kama Yehova Mungu wetu,+Yeye anayefanya makao yake juu?+
6 Yeye anajishusha kutazama mbingu na dunia,+
7 Akimwinua mtu wa hali ya chini kutoka kwenye mavumbi;+Humwinua maskini kutoka kwenye shimo la majivu,+
8 Ili kumketisha pamoja na wenye vyeo,+Wenye vyeo kati ya watu wake.+
9 Anampa mwanamke tasa makao katika nyumba+Kama mama ya wana aliye na shangwe.+Msifuni Yah!+