Yohana 17:1-26
17 Yesu alisema mambo haya, akainua macho yake mbinguni,+ akasema: “Baba, saa imefika; mtukuze mwana wako, ili mwana wako apate kukutukuza wewe,+
2 kulingana na vile ambavyo umempa mamlaka juu ya wote wenye mwili,+ ili, wote ambao umempa,+ yeye apate kuwapa uzima wa milele.+
3 Uzima wa milele+ ndio huu, waendelee kupata ujuzi+ juu yako wewe, Mungu wa pekee wa kweli,+ na juu ya yule uliyemtuma, Yesu Kristo.+
4 Nimekutukuza+ duniani, nikiwa nimemaliza kazi ambayo umenipa niifanye.+
5 Kwa hiyo sasa wewe, Baba, nitukuze kando yako kwa utukufu niliokuwa nao kando yako kabla ya ulimwengu kuwako.+
6 “Nimelifunua jina lako kwa watu ulionipa kutoka ulimwenguni.+ Walikuwa wako, nawe ukanipa, nao wamelishika neno lako.
7 Sasa wamejua kwamba yote uliyonipa yametoka kwako;
8 kwa sababu maneno uliyonipa nimewapa, nao wameyapokea+ na wamejua kwamba nilitoka nikiwa mwakilishi+ wako, nao wameamini kwamba ulinituma.+
9 Ninaomba juu yao; ninawaombea hao, siuombei ulimwengu,+ bali ninawaombea wale ambao umenipa; kwa sababu ni wako,
10 na vitu vyangu vyote ni vyako na vyako ni vyangu,+ nami nimetukuzwa kati yao.
11 “Pia, mimi simo tena ulimwenguni, bali wao wamo ulimwenguni+ nami ninakuja kwako. Baba Mtakatifu, walinde+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa, ili wawe kitu kimoja kama vile sisi tulivyo.+
12 Nilipokuwa pamoja nao nilikuwa nikiwalinda+ kwa sababu ya jina lako ambalo umenipa; nami nimewatunza, na hata mmoja wao hakuangamizwa+ ila yule mwana wa maangamizi,+ ili andiko lipate kutimizwa.+
13 Lakini sasa ninakuja kwako, nami ninasema mambo haya ulimwenguni ili wao wapate kuwa na shangwe yangu ndani yao wenyewe kwa ukamili.+
14 Nimewapa neno lako, lakini ulimwengu umewachukia,+ kwa sababu wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.+
15 “Ninakuomba, si kwamba uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde kwa sababu ya yule mwovu.+
16 Wao si sehemu ya ulimwengu,+ kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.+
17 Watakase+ kwa njia ya ile kweli; neno+ lako ni kweli.+
18 Kama vile ulivyonituma ulimwenguni, vivyo hivyo mimi pia nimewatuma ulimwenguni.+
19 Nami ninajitakasa kwa ajili yao, ili wao pia watakaswe+ kwa njia ya ile kweli.
20 “Ninawaombea, si hawa tu, bali pia wale wanaoniamini kupitia neno lao;+
21 ili wote wapate kuwa kitu kimoja,+ kama vile ambavyo wewe, Baba, umo katika muungano pamoja na mimi na mimi nimo katika muungano pamoja na wewe,+ ili wao pia wapate kuwa katika muungano pamoja na sisi,+ ili ulimwengu upate kuamini kwamba ulinituma.+
22 Pia, nimewapa utukufu ambao umenipa, ili wapate kuwa kitu kimoja kama vile sisi tulivyo kitu kimoja.+
23 Mimi katika muungano pamoja na wao na wewe katika muungano pamoja na mimi, ili wapate kukamilishwa kuwa kitu kimoja,+ ili ulimwengu upate kujua kwamba wewe ulinituma na kwamba uliwapenda wao kama vile ulivyonipenda mimi.
24 Baba, kwa habari ya kile ambacho umenipa, ninataka kwamba, mahali nilipo, wao pia wapate kuwa pamoja nami,+ ili wauone utukufu wangu ambao umenipa, kwa sababu ulinipenda kabla ya kuwekwa kwa msingi+ wa ulimwengu.+
25 Baba Mwadilifu,+ kwa kweli, ulimwengu haujakujua wewe;+ lakini mimi nimekujua, na hawa wamejua kwamba ulinituma.+
26 Nami nimewajulisha+ jina lako nami nitalijulisha, ili upendo ulionipenda nao upate kuwa ndani yao nami katika muungano pamoja nao.”+