Waroma 3:1-31
3 Basi, Myahudi+ ana ubora gani, au ni nini faida ya kutahiriwa?+
2 Ni nyingi katika kila njia. Kwanza kabisa, kwa sababu wao walikabidhiwa maneno matakatifu ya Mungu.+
3 Basi, hali ikoje? Ikiwa wengine hawakuonyesha imani,+ je, ukosefu wao wa imani labda utafanya uaminifu+ wa Mungu usiwe na matokeo?+
4 Hilo lisitendeke kamwe! Bali Mungu na aonekane kuwa wa kweli,+ ingawa kila mwanadamu aonekane kuwa mwongo,+ kama ilivyoandikwa: “Ili uonekane kuwa mwadilifu katika maneno yako na ushinde wakati unapohukumiwa.”+
5 Hata hivyo, ikiwa ukosefu wetu wa uadilifu unatokeza wazi uadilifu+ wa Mungu, tutasema nini? Je, Mungu hukosa haki+ anapofungulia ghadhabu yake? (Ninasema kama mwanadamu+ anavyosema.)
6 Hilo lisitendeke kamwe! Ikiwa hivyo, Mungu atauhukumu ulimwengu jinsi gani?+
7 Lakini ikiwa kwa sababu ya uwongo wangu kweli ya Mungu+ imefanywa ionekane wazi zaidi kwa utukufu wake, kwa nini bado mimi pia ninahukumiwa kuwa mtenda-dhambi?+
8 Na kwa nini isisemwe, kama tunavyoshtakiwa kwa uwongo+ na kama watu fulani wanavyosema kuwa sisi husema: “Na tufanye mambo mabaya ili mambo mema yaje”?+ Hukumu+ juu ya watu hao inapatana na haki.+
9 Tuseme nini basi? Je, sisi tuna hali bora?+ Sivyo hata kidogo! Kwa maana hapo juu tumefanya shtaka kwamba Wayahudi na vilevile Wagiriki wote wako chini ya dhambi;+
10 kama ilivyoandikwa: “Hakuna mwanadamu mwadilifu, hakuna hata mmoja;+
11 hakuna yeyote aliye na ufahamu wowote, hakuna yeyote anayemtafuta Mungu.+
12 Watu wote wamepotoka, wote pamoja wamekuwa wasiofaa kitu; hakuna yeyote anayetenda fadhili, hakuna hata mmoja.”+
13 “Koo yao ni kaburi lililo wazi, wamedanganya kwa ndimi zao.”+ “Sumu ya nyoka iko nyuma ya midomo yao.”+
14 “Na kinywa chao kimejaa kulaani na maneno machungu.”+
15 “Miguu yao inaharakisha kwenda kumwaga damu.”+
16 “Uharibifu na taabu zimo katika njia zao,+
17 nao hawajaijua njia ya amani.”+
18 “Hakuna kumwogopa Mungu mbele ya macho yao.”+
19 Sasa tunajua kwamba mambo yote ambayo Sheria+ inasema, inawaambia wale walio chini ya Sheria, ili kila kinywa kizibwe+ na ulimwengu wote ustahili+ adhabu kutoka kwa Mungu.+
20 Kwa hiyo hakuna mwili wowote utakaotangazwa kuwa mwadilifu+ kutokana na matendo ya sheria+ mbele zake, kwa maana ujuzi sahihi juu ya dhambi ni kwa njia ya sheria.+
21 Lakini sasa uadilifu+ wa Mungu umefunuliwa bila sheria, kama unavyotolewa ushahidi+ na Sheria+ na Manabii;+
22 ndiyo, uadilifu wa Mungu kupitia imani katika Yesu Kristo,+ kwa ajili ya wote walio na imani.+ Kwa maana hakuna tofauti.+
23 Kwa maana wote wamefanya dhambi+ na kupungukiwa na utukufu wa Mungu,+
24 nayo ni zawadi ya bure+ kwamba wanatangazwa kuwa waadilifu kwa fadhili zake zisizostahiliwa+ kupitia kuachiliwa huru kwa njia ya fidia+ ambayo Kristo Yesu alilipa.
25 Mungu alimweka kuwa toleo la kupatanisha+ kupitia imani katika damu+ yake. Ilikuwa hivyo ili kuonyesha wazi uadilifu wake mwenyewe, kwa sababu alikuwa akizisamehe dhambi+ zilizotokea wakati uliopita wakati Mungu alipokuwa akivumilia kwa subira;+
26 ili kuonyesha wazi uadilifu+ wake mwenyewe katika majira haya yaliyopo, ili awe mwadilifu hata anapomtangaza kuwa mwadilifu+ mtu aliye na imani katika Yesu.
27 Basi, kujisifu+ kuko wapi? Kumefungiwa nje. Kupitia sheria+ gani? Ile ya matendo?+ Hapana, bali kupitia sheria ya imani.+
28 Kwa maana tunaamua kwamba mtu hutangazwa kuwa mwadilifu kwa imani bila matendo ya sheria.+
29 Au je, yeye ni Mungu wa Wayahudi peke yao?+ Je, yeye si wa watu wa mataifa pia?+ Ndiyo, wa watu wa mataifa pia,+
30 ikiwa kwa kweli Mungu ni mmoja,+ atakayewatangaza watu waliotahiriwa+ kuwa waadilifu kutokana na imani na watu wasiotahiriwa+ kuwa waadilifu kwa njia ya imani yao.
31 Basi, je, tunaifuta sheria kupitia imani yetu?+ Hilo lisitendeke kamwe! Kinyume cha hilo, sisi tunaiimarisha sheria.+