Waroma 14:1-23
14 Mkaribisheni mtu aliye na udhaifu+ katika imani yake, lakini msifanye maamuzi juu ya maswali ya ndani.+
2 Mtu mmoja ana imani ya kula kila kitu,+ lakini mtu aliye dhaifu hula mboga za majani.
3 Yeye anayekula asimdharau yeye asiyekula,+ na yeye asiyekula asimhukumu yeye anayekula, kwa maana Mungu amemkaribisha huyo.
4 Wewe ni nani ili umhukumu mtumishi wa nyumbani wa mwingine?+ Kwa bwana wake mwenyewe yeye husimama au kuanguka.+ Kwa kweli, atasimamishwa, kwa maana Yehova anaweza kumsimamisha. +
5 Mtu mmoja anahukumu siku moja kuwa juu ya nyingine;+ mtu mwingine anahukumu siku moja kuwa kama nyingine zote;+ kila mtu na asadikishwe kikamili katika akili yake mwenyewe.
6 Yeye anayeishika siku huishika kwa ajili ya Yehova. Pia, yeye anayekula, anakula kwa ajili ya Yehova,+ kwa maana yeye humshukuru Mungu;+ na yeye asiyekula hali chakula kwa ajili ya Yehova,+ na bado yeye humshukuru Mungu.+
7 Kwa kweli, hakuna hata mmoja wetu anayeishi kwa ajili yake mwenyewe tu,+ na hakuna yeyote anayekufa kwa ajili yake mwenyewe tu;
8 kwa maana tukiishi, tunaishi kwa ajili ya Yehova,+ na tukifa, tunakufa kwa ajili ya Yehova.+ Kwa hiyo tukiishi na tukifa, sisi ni wa Yehova.+
9 Kwa maana kwa kusudi hili Kristo alikufa na kuwa hai tena,+ ili awe Bwana juu ya waliokufa+ na walio hai+ pia.
10 Lakini kwa nini wewe unamhukumu ndugu yako?+ Au kwa nini wewe pia unamdharau ndugu yako? Kwa maana sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu+ cha Mungu;
11 kwa maana imeandikwa: “ ‘Kama ninavyoishi,’ asema Yehova,+ ‘kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utakiri waziwazi kwa Mungu.’ ”+
12 Hivyo, basi, kila mmoja wetu atatoa hesabu kwa Mungu kwa ajili yake mwenyewe.+
13 Kwa hiyo sisi na tusiwe tukihukumiana+ tena, bali badala yake fanyeni hili kuwa uamuzi+ wenu, kutokuweka mbele ya ndugu+ kikwazo+ au sababu ya kujikwaa.
14 Najua nami nasadikishwa katika Bwana Yesu kwamba hakuna kitu ambacho ndani yake chenyewe ni najisi;+ ni pale tu ambapo mtu anakiona kitu kuwa najisi, kwake yeye hicho huwa najisi.+
15 Kwa maana ikiwa ndugu yako anahuzunishwa kwa sababu ya chakula, wewe hutembei tena kupatana na upendo.+ Kwa chakula chako usimwangamize yule ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.+
16 Kwa hiyo, msiache msemwe vibaya kwa mema mnayofanya.
17 Kwa maana ufalme wa Mungu+ haumaanishi kula na kunywa,+ bali unamaanisha uadilifu+ na amani+ na shangwe+ pamoja na roho takatifu.
18 Kwa maana yeye ambaye kwa habari hii anamtumikia Kristo anakubalika kwa Mungu naye ana kibali cha wanadamu.+
19 Hivyo, basi, na tufuatilie mambo yanayofanya kuwe na amani+ na mambo ambayo ni ya kujengana.+
20 Acheni kuibomoa kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula+ tu. Ni kweli, vitu vyote ni safi, lakini ni jambo baya kwa mtu ambaye hula kukiwa na hali ya kukwaza.+
21 Ni vema kutokula nyama au kunywa divai au kufanya jambo lolote ambalo ndugu yako anakwazika juu yake.+
22 Imani uliyo nayo, uwe nayo kupatana na wewe mwenyewe machoni pa Mungu.+ Mwenye furaha ni mtu asiyejitia mwenyewe hukumuni kwa yale anayokubali.
23 Lakini ikiwa ana shaka, yeye akila tayari atakuwa amehukumiwa kuwa mwenye hatia,+ kwa sababu hali kwa imani. Kwa kweli, kila kitu ambacho hakitokani na imani ni dhambi.+