Waroma 10:1-21

10  Akina ndugu, nia njema ya moyo wangu na dua yangu kwa Mungu kwa ajili yao, kwa kweli, ni kwa ajili ya wokovu wao.+  Kwa maana nawatolea ushahidi kwamba wana bidii+ kwa ajili ya Mungu; lakini si kulingana na ujuzi sahihi;+  kwa maana, kwa sababu ya kukosa kujua uadilifu wa Mungu+ bali wakitafuta kujiwekea uadilifu wao wenyewe,+ hawakujitiisha kwa uadilifu wa Mungu.+  Kwa maana Kristo ndiye mwisho wa Sheria,+ ili kila mtu anayeonyesha imani awe na uadilifu.+  Kwa maana Musa anaandika kwamba mtu ambaye amefanya uadilifu wa Sheria ataishi kwa huo.+  Lakini uadilifu unaotokana na imani husema kwa namna hii: “Usiseme moyoni mwako,+ ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’+ yaani, kumleta Kristo+ chini;  au, ‘Ni nani atakayeshuka katika abiso?’+ yaani, kumleta Kristo juu kutoka kwa wafu.”+  Lakini linasema nini? “Lile neno liko karibu nawe, katika kinywa chako mwenyewe na katika moyo wako mwenyewe”;+ yaani, “neno”+ la imani, ambalo sisi tunahubiri.+  Kwa maana ukitangaza waziwazi lile ‘neno lililo katika kinywa chako mwenyewe,’+ kwamba Yesu ni Bwana,+ na kuonyesha imani moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu,+ utaokolewa.+ 10  Kwa maana kwa moyo+ mtu huonyesha imani kwa ajili ya uadilifu, lakini kwa kinywa mtu hufanya tangazo la hadharani+ kwa ajili ya wokovu. 11  Kwa maana Andiko linasema: “Yeyote anayemwamini+ hatakata tamaa.”+ 12  Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Mgiriki,+ kwa maana kuna Bwana yuleyule juu ya wote, aliye tajiri+ kwa wale wote wanaomwitia. 13  Kwa maana “kila mtu anayeliitia jina la Yehova ataokolewa.”+ 14  Hata hivyo, watawezaje kumwitia yeye ambaye hawajamwamini?+ Nao watamwaminije yeye ambaye hawajamsikia? Nao watasikiaje bila mtu wa kuhubiri?+ 15  Nao watahubirije isipokuwa wawe wametumwa?+ Kama ilivyoandikwa: “Jinsi ilivyo yenye kupendeza miguu ya wale wanaotangaza habari njema ya mambo mema!”+ 16  Hata hivyo, si wote waliotii habari njema.+ Kwa maana Isaya anasema: “Yehova, ni nani aliyeliamini jambo ambalo limesikiwa kutoka kwetu?”+ 17  Kwa hiyo imani hufuata jambo lililosikiwa.+ Nalo jambo lililosikiwa ni kupitia neno kumhusu Kristo.+ 18  Hata hivyo nauliza, Je, walikosa kusikia? Kwani, kwa kweli, “sauti yao ilifika+ katika dunia yote, na maneno yao mpaka miisho ya dunia inayokaliwa.”+ 19  Hata hivyo, nauliza, je, Israeli walikosa kujua?+ Kwanza Musa anasema: “Nitawachochea ninyi kuwa na wivu kupitia lile ambalo si taifa; nitawachochea ninyi kuwa na hasira kali kupitia taifa jinga.”+ 20  Lakini Isaya anakuwa mjasiri sana na kusema: “Wale ambao hawakuwa wakinitafuta walinipata;+ nikajifunua kwa wale ambao hawakuwa wakiuliza juu yangu.”+ 21  Lakini kwa habari ya Israeli yeye anasema: “Mchana kutwa nimewanyooshea mikono yangu watu wasiotii+ na wanaojibu kwa ujeuri.”+

Maelezo ya Chini