Waroma 1:1-32

1  Paulo, mtumwa+ wa Yesu Kristo aliyeitwa+ kuwa mtume,+ aliyetengwa kwa ajili ya habari njema ya Mungu,+  aliyoahidi kimbele kupitia manabii+ wake katika Maandiko matakatifu,  kuhusu Mwana wake, aliyetokana na uzao wa Daudi+ kulingana na mwili,+  lakini ambaye kwa nguvu+ alitangazwa kuwa Mwana wa Mungu+ kulingana na roho+ ya utakatifu kwa njia ya ufufuo kutoka kwa wafu+—ndiyo, Yesu Kristo Bwana wetu,  ambaye kupitia yeye tulipokea fadhili zisizostahiliwa+ na utume+ ili kuwe na utii wa imani kati ya mataifa+ yote kuhusu jina lake,  mataifa ambayo kati yake ninyi pia ni wale walioitwa kuwa wa Yesu Kristo—  kwa wale wote walio katika Roma wakiwa wapendwa wa Mungu, walioitwa+ wawe watakatifu:+ Na muwe na fadhili zisizostahiliwa na amani+ kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana Yesu Kristo.+  Kwanza kabisa, namshukuru+ Mungu wangu kupitia Yesu Kristo kuhusu ninyi nyote, kwa sababu imani yenu inazungumzwa+ kotekote ulimwenguni.  Kwa maana Mungu, ambaye ninamtolea utumishi mtakatifu kwa roho yangu kuhusiana na ile habari njema juu ya Mwana wake, ni shahidi+ wangu wa jinsi ninavyowataja sikuzote katika sala zangu bila kuacha,+ 10  nikiomba kwamba ikiwa kwa vyovyote inawezekana sasa mwishowe nipate kufanikiwa katika mapenzi+ ya Mungu ili nije kwenu. 11  Kwa maana ninatamani kuwaona ninyi,+ ili niwape sehemu ya zawadi ya kiroho+ kusudi mfanywe imara; 12  au, badala ya hivyo, kwamba kuwe na ubadilishanaji wa kitia-moyo kati yenu,+ kila mmoja kupitia imani ya mwingine,+ yenu na yangu pia. 13  Lakini, akina ndugu,+ sitaki mkose kujua kwamba mara nyingi nilikusudia kuja kwenu+ ili niweze kujipatia matunda fulani+ kati yenu pia kama vile ilivyo kati ya mataifa mengine, lakini nimezuiwa mpaka sasa. 14  Mimi nina deni kwa Wagiriki na kwa Wabaribari pia, kwa wenye hekima+ na kwa wasio na akili pia: 15  kwa hiyo nina hamu ya kuitangaza habari njema+ kwenu pia mlio huko Roma.+ 16  Kwa maana siionei aibu+ habari njema; kwa kweli, hiyo ni nguvu za Mungu+ kwa ajili ya wokovu kwa kila mtu aliye na imani,+ kwa Myahudi kwanza+ na pia kwa Mgiriki;+ 17  kwa maana katika hiyo uadilifu+ wa Mungu unafunuliwa kwa sababu ya imani+ na kuelekea imani, kama vile ilivyoandikwa: “Lakini mwadilifu—ataishi kwa njia ya imani.”+ 18  Kwa maana ghadhabu+ ya Mungu inafunuliwa kutoka mbinguni juu ya watu wote wasiomwogopa Mungu na wasio waadilifu+ ambao wanaikandamiza kweli+ katika njia isiyo ya uadilifu,+ 19  kwa sababu yale yanayoweza kujulikana juu ya Mungu yamefunuliwa katikati yao,+ kwa maana Mungu aliyafunua kwao.+ 20  Kwa maana sifa zake ambazo hazionekani,+ zinaonekana waziwazi tangu kuumbwa kwa ulimwengu na kuendelea,+ kwa sababu zinaeleweka kwa vitu vilivyofanywa,+ yaani, nguvu zake za milele+ na Uungu,+ hivi kwamba hawana sababu ya kujitetea.+ 21  Kwa sababu, ijapokuwa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kuwa Mungu wala hawakumshukuru,+ bali wakawa wajinga+ katika kufikiri kwao na moyo wao usio na ufahamu ukaingiwa na giza.+ 22  Ijapokuwa walisisitiza kuwa ni wenye hekima, wakawa wapumbavu+ 23  na kuugeuza utukufu+ wa Mungu asiye na uharibifu kuwa kitu kama sanamu+ ya mwanadamu aliye na uharibifu na ya ndege na viumbe vyenye miguu minne na vitu vinavyotambaa.+ 24  Kwa hiyo, kwa kupatana na tamaa za mioyo yao, Mungu aliwaacha katika uchafu,+ ili miili+ yao ivunjiwe heshima kati yao,+ 25  yaani, wale walioibadili kweli+ ya Mungu kwa ajili ya uwongo+ nao wakauheshimu mno uumbaji na kuutolea utumishi mtakatifu badala ya kumtolea Yeye aliyeumba, anayebarikiwa milele. Amina. 26  Ndiyo sababu Mungu aliwaacha katika hamu za ngono yenye kufedhehesha,+ kwa maana wanawake wao walibadili matumizi yao wenyewe ya asili kuwa yale yaliyo kinyume cha asili;+ 27  na vivyo hivyo pia hata wanaume waliacha matumizi ya asili ya mwanamke+ na kuwakiana tamaa kali katika uchu wao kuelekeana wao wenyewe, wanaume kwa wanaume,+ wakitenda mambo machafu+ na kupokea ndani yao wenyewe malipo kamili,+ yaliyostahili kosa lao.+ 28  Na kama vile ambavyo hawakukubali kumjua Mungu katika ujuzi sahihi,+ Mungu aliwaacha katika hali ya akili iliyokataliwa,+ ili wafanye mambo yasiyofaa,+ 29  wakiwa wamejawa na ukosefu wote wa uadilifu,+ uovu,+ tamaa,+ ubaya,+ wakiwa wamejaa wivu,+ uuaji,+ mizozo,+ udanganyifu,+ mwelekeo wenye madhara,+ wakiwa wanong’onezaji,+ 30  wasengenyaji,+ wenye kumchukia Mungu, wenye dharau,+ wenye majivuno,+ wenye kujidai,+ wenye kutunga mambo mabaya,+ wasiotii wazazi,+ 31  wasio na uelewaji,+ waongo kwa mapatano,+ wasio na upendo wa asili,+ wasio na rehema.+ 32  Ijapokuwa hawa wanajua vema kabisa amri ya uadilifu ya Mungu,+ kwamba wale wanaozoea kufanya mambo ya namna hiyo wanastahili kifo,+ wao wanaendelea kuyafanya na vilevile hukubaliana+ na wale wanaozoea kuyafanya.

Maelezo ya Chini