Methali 30:1-33

30  Maneno ya Aguri mwana wa Yake, ujumbe mzito.+ Maneno ya huyo mwanamume aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.  Kwa maana mimi nawapita watu wote kwa kutotumia akili,+ nami sina ule uelewaji wa wanadamu;+  na sijajifunza hekima;+ nao ujuzi wa Aliye Mtakatifu Zaidi siujui.+  Ni nani ambaye amepanda mbinguni ili apate kushuka?+ Ni nani ambaye amekusanya upepo+ katika makonzi yake mawili? Ni nani ambaye ameyafunga maji ndani ya nguo ya kujitanda?+ Ni nani ambaye amefanya miisho yote ya dunia iinuke?+ Jina lake ni nani+ nalo jina la mwana wake ni nani, ikiwa unajua?+  Kila neno la Mungu ni safi.+ Yeye ni ngao kwao wanaomkimbilia.+  Usiongeze chochote katika maneno yake+ asije akakukaripia, wala usionekane kuwa mwongo.+  Nimeomba mambo mawili kutoka kwako.+ Usininyime mambo hayo kabla sijafa.+  Maneno yasiyo ya kweli na ya uwongo uyaondolee mbali nami.+ Usinipe umaskini wala utajiri.+ Acha nile chakula nilichoamriwa,+  nisije nikashiba nikakukana,+ nikasema: “Yehova ni nani?”+ wala nisiwe maskini, nikaiba na kulishambulia jina la Mungu wangu.+ 10  Usimchongee mtumishi kwa bwana wake,+ asije akakulaani, nawe usihesabiwe kuwa na hatia.+ 11  Kuna kizazi cha watu ambao humlaani hata baba yao wala hawambariki hata mama yao.+ 12  Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao+ wenyewe lakini ambao bado hawajaoshwa mavi yao.+ 13  Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yamekwezwa kama nini! na ambao macho yao yenye kung’aa yameinuliwa.+ 14  Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga na ambao mifupa yao ya taya ni visu vya kuchinjia,+ ili kuwala wenye kuteseka waondolewe duniani na maskini watoke kati ya wanadamu.+ 15  Wadudu-ruba wana binti wawili wanaolia: “Nipe! Nipe!” Kuna vitu vitatu visivyoshiba, naam, kuna vinne ambavyo havijasema: “Inatosha!” 16  Kaburi*+ na tumbo la uzazi lililozuiwa,+ nchi ambayo haijashiba maji,+ na moto+ usiosema: “Inatosha!”+ 17  Jicho ambalo humdhihaki baba na kudharau utii kwa mama+—kunguru wa bondeni wataling’oa na wana wa tai watalila. 18  Kuna mambo matatu ambayo yameonekana kuwa ya ajabu mno kwangu, naam, kuna manne ambayo sijapata kuyajua: 19  njia ya tai mbinguni, njia ya nyoka juu ya mwamba, njia ya meli katika moyo wa bahari+ na njia ya mwanamume pamoja na mwanamwali.+ 20  Tazama, hii ndiyo njia ya mwanamke mzinzi: amekula, akapangusa kinywa chake na kusema: “Sijafanya kosa lolote.”+ 21  Chini ya mambo matatu dunia imehangaishwa, na chini ya manne haiwezi kuvumilia: 22  chini ya mtumwa anapotawala akiwa mfalme,+ na mtu asiye na akili anapokuwa na chakula cha kutosha;+ 23  chini ya mwanamke anayechukiwa wakati anapochukuliwa na kuwa mke,+ na mjakazi anapompindua bimkubwa wake.+ 24  Kuna vitu vinne vilivyo vidogo zaidi duniani, lakini vina hekima ya kisilika:+ 25  chungu ni kikundi cha watu wasio na nguvu,+ hata hivyo wakati wa kiangazi wao hutayarisha chakula chao;+ 26  wibari+ ni kikundi cha watu wasio na nguvu, hata hivyo wao hujenga nyumba yao kwenye mwamba;+ 27  nzige+ hawana mfalme, hata hivyo wao huenda mbele wote wakiwa wamegawanywa vikundi-vikundi;+ 28  mjusi+ hushika kwa mikono yake mwenyewe naye yumo katika jumba kuu la mfalme. 29  Kuna watatu wenye mwendo mzuri, na kuna wanne wanaotembea vyema: 30  simba, ambaye ndiye mwenye nguvu zaidi kati ya wanyama na wala harudi nyuma mbele ya yeyote;+ 31  mbwa-mwindaji au mbuzi-dume, na mfalme wa kikosi cha askari-jeshi cha watu wake mwenyewe.+ 32  Ikiwa umetenda bila kutumia akili kwa kujiinua mwenyewe,+ na ikiwa umekaza fikira zako juu ya jambo hilo, weka mkono wako kwenye kinywa chako.+ 33  Kwa maana kupiga-piga maziwa ndiko hutokeza siagi, na kufinya pua ndiko hutokeza damu, na kuchochea hasira ndiko hutokeza ugomvi.+

Maelezo ya Chini

Sheoli. Tazama Nyongeza 4.