Methali 30:1-33
30 Maneno ya Aguri mwana wa Yake, ujumbe mzito.+ Maneno ya huyo mwanamume aliyomwambia Ithieli, naam, Ithieli na Ukali.
2 Kwa maana mimi nawapita watu wote kwa kutotumia akili,+ nami sina ule uelewaji wa wanadamu;+
3 na sijajifunza hekima;+ nao ujuzi wa Aliye Mtakatifu Zaidi siujui.+
4 Ni nani ambaye amepanda mbinguni ili apate kushuka?+ Ni nani ambaye amekusanya upepo+ katika makonzi yake mawili? Ni nani ambaye ameyafunga maji ndani ya nguo ya kujitanda?+ Ni nani ambaye amefanya miisho yote ya dunia iinuke?+ Jina lake ni nani+ nalo jina la mwana wake ni nani, ikiwa unajua?+
5 Kila neno la Mungu ni safi.+ Yeye ni ngao kwao wanaomkimbilia.+
6 Usiongeze chochote katika maneno yake+ asije akakukaripia, wala usionekane kuwa mwongo.+
7 Nimeomba mambo mawili kutoka kwako.+ Usininyime mambo hayo kabla sijafa.+
8 Maneno yasiyo ya kweli na ya uwongo uyaondolee mbali nami.+ Usinipe umaskini wala utajiri.+ Acha nile chakula nilichoamriwa,+
9 nisije nikashiba nikakukana,+ nikasema: “Yehova ni nani?”+ wala nisiwe maskini, nikaiba na kulishambulia jina la Mungu wangu.+
10 Usimchongee mtumishi kwa bwana wake,+ asije akakulaani, nawe usihesabiwe kuwa na hatia.+
11 Kuna kizazi cha watu ambao humlaani hata baba yao wala hawambariki hata mama yao.+
12 Kuna kizazi cha watu walio safi machoni pao+ wenyewe lakini ambao bado hawajaoshwa mavi yao.+
13 Kuna kizazi cha watu ambao macho yao yamekwezwa kama nini! na ambao macho yao yenye kung’aa yameinuliwa.+
14 Kuna kizazi cha watu ambao meno yao ni panga na ambao mifupa yao ya taya ni visu vya kuchinjia,+ ili kuwala wenye kuteseka waondolewe duniani na maskini watoke kati ya wanadamu.+
15 Wadudu-ruba wana binti wawili wanaolia: “Nipe! Nipe!” Kuna vitu vitatu visivyoshiba, naam, kuna vinne ambavyo havijasema: “Inatosha!”
16 Kaburi*+ na tumbo la uzazi lililozuiwa,+ nchi ambayo haijashiba maji,+ na moto+ usiosema: “Inatosha!”+
17 Jicho ambalo humdhihaki baba na kudharau utii kwa mama+—kunguru wa bondeni wataling’oa na wana wa tai watalila.
18 Kuna mambo matatu ambayo yameonekana kuwa ya ajabu mno kwangu, naam, kuna manne ambayo sijapata kuyajua:
19 njia ya tai mbinguni, njia ya nyoka juu ya mwamba, njia ya meli katika moyo wa bahari+ na njia ya mwanamume pamoja na mwanamwali.+
20 Tazama, hii ndiyo njia ya mwanamke mzinzi: amekula, akapangusa kinywa chake na kusema: “Sijafanya kosa lolote.”+
21 Chini ya mambo matatu dunia imehangaishwa, na chini ya manne haiwezi kuvumilia:
22 chini ya mtumwa anapotawala akiwa mfalme,+ na mtu asiye na akili anapokuwa na chakula cha kutosha;+
23 chini ya mwanamke anayechukiwa wakati anapochukuliwa na kuwa mke,+ na mjakazi anapompindua bimkubwa wake.+
24 Kuna vitu vinne vilivyo vidogo zaidi duniani, lakini vina hekima ya kisilika:+
25 chungu ni kikundi cha watu wasio na nguvu,+ hata hivyo wakati wa kiangazi wao hutayarisha chakula chao;+
26 wibari+ ni kikundi cha watu wasio na nguvu, hata hivyo wao hujenga nyumba yao kwenye mwamba;+
27 nzige+ hawana mfalme, hata hivyo wao huenda mbele wote wakiwa wamegawanywa vikundi-vikundi;+
28 mjusi+ hushika kwa mikono yake mwenyewe naye yumo katika jumba kuu la mfalme.
29 Kuna watatu wenye mwendo mzuri, na kuna wanne wanaotembea vyema:
30 simba, ambaye ndiye mwenye nguvu zaidi kati ya wanyama na wala harudi nyuma mbele ya yeyote;+
31 mbwa-mwindaji au mbuzi-dume, na mfalme wa kikosi cha askari-jeshi cha watu wake mwenyewe.+
32 Ikiwa umetenda bila kutumia akili kwa kujiinua mwenyewe,+ na ikiwa umekaza fikira zako juu ya jambo hilo, weka mkono wako kwenye kinywa chako.+
33 Kwa maana kupiga-piga maziwa ndiko hutokeza siagi, na kufinya pua ndiko hutokeza damu, na kuchochea hasira ndiko hutokeza ugomvi.+
Maelezo ya Chini
^ Sheoli. Tazama Nyongeza 4.