Methali 2:1-22
2 Mwanangu, ikiwa utapokea maneno yangu+ na kujiwekea amri zangu kama hazina,+
2 ili kwa sikio lako usikilize hekima kwa makini,+ ili uelekeze moyo wako kwenye utambuzi,+
3 ikiwa utaita uelewaji+ na kupaaza sauti yako uite utambuzi,+
4 ikiwa utaendelea kuutafuta kama fedha,+ na kuendelea kuutafuta kama hazina zilizofichika,+
5 ndipo utakapoelewa kumwogopa+ Yehova, nawe utapata kumjua Mungu.+
6 Kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima;+ kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.+
7 Naye atawawekea wanyoofu hazina ya hekima inayotumika;+ yeye ni ngao kwa wale wanaotembea kwa utimilifu,+
8 kwa kushika mapito ya hukumu,+ naye atailinda njia ya washikamanifu wake.+
9 Ndipo utakapoelewa uadilifu na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.+
10 Hekima inapoingia moyoni mwako+ na ujuzi kupendeza nafsi yako,+
11 uwezo wa kufikiri utakutunza,+ utambuzi utakulinda,+
12 ili kukukomboa kutoka katika njia mbaya,+ na kutoka kwa mtu anayesema mambo mapotovu,+
13 kutoka kwa wale wanaoacha mapito ya unyoofu ili watembee katika njia za giza,+
14 kutoka kwa wale wanaofurahia kufanya mabaya,+ wanaoshangilia mambo mapotovu ya ubaya;+
15 wale ambao mapito yao yamepotoka na ambao kwa ujumla ni wenye hila maishani mwao;+
16 ili huo ukukomboe kutoka kwa mwanamke, naam, kutoka kwa mwanamke mgeni+ ambaye amefanya maneno yake kuwa laini,+
17 anayemwacha rafiki wa ujana wake+ na ambaye amelisahau agano la Mungu wake.+
18 Kwa maana nyumba yake huzama ndani ya kifo na mapito yake huzama ndani kwa wale wasiojiweza katika kifo.+
19 Hakuna yeyote kati ya wale wanaolala naye atakayerudi, wala hawatayafikia tena mapito ya walio hai.+
20 Kusudi ni kwamba upate kutembea katika njia ya watu wema+ na kwamba upate kushika mapito ya waadilifu.+
21 Kwa maana wanyoofu ndio watakaokaa duniani,+ na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake.+
22 Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani;+ nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.+