Methali 2:1-22

2  Mwanangu, ikiwa utapokea maneno yangu+ na kujiwekea amri zangu kama hazina,+  ili kwa sikio lako usikilize hekima kwa makini,+ ili uelekeze moyo wako kwenye utambuzi,+  ikiwa utaita uelewaji+ na kupaaza sauti yako uite utambuzi,+  ikiwa utaendelea kuutafuta kama fedha,+ na kuendelea kuutafuta kama hazina zilizofichika,+  ndipo utakapoelewa kumwogopa+ Yehova, nawe utapata kumjua Mungu.+  Kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima;+ kinywani mwake hutoka ujuzi na utambuzi.+  Naye atawawekea wanyoofu hazina ya hekima inayotumika;+ yeye ni ngao kwa wale wanaotembea kwa utimilifu,+  kwa kushika mapito ya hukumu,+ naye atailinda njia ya washikamanifu wake.+  Ndipo utakapoelewa uadilifu na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.+ 10  Hekima inapoingia moyoni mwako+ na ujuzi kupendeza nafsi yako,+ 11  uwezo wa kufikiri utakutunza,+ utambuzi utakulinda,+ 12  ili kukukomboa kutoka katika njia mbaya,+ na kutoka kwa mtu anayesema mambo mapotovu,+ 13  kutoka kwa wale wanaoacha mapito ya unyoofu ili watembee katika njia za giza,+ 14  kutoka kwa wale wanaofurahia kufanya mabaya,+ wanaoshangilia mambo mapotovu ya ubaya;+ 15  wale ambao mapito yao yamepotoka na ambao kwa ujumla ni wenye hila maishani mwao;+ 16  ili huo ukukomboe kutoka kwa mwanamke, naam, kutoka kwa mwanamke mgeni+ ambaye amefanya maneno yake kuwa laini,+ 17  anayemwacha rafiki wa ujana wake+ na ambaye amelisahau agano la Mungu wake.+ 18  Kwa maana nyumba yake huzama ndani ya kifo na mapito yake huzama ndani kwa wale wasiojiweza katika kifo.+ 19  Hakuna yeyote kati ya wale wanaolala naye atakayerudi, wala hawatayafikia tena mapito ya walio hai.+ 20  Kusudi ni kwamba upate kutembea katika njia ya watu wema+ na kwamba upate kushika mapito ya waadilifu.+ 21  Kwa maana wanyoofu ndio watakaokaa duniani,+ na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake.+ 22  Nao waovu, watakatiliwa mbali kutoka duniani;+ nao wenye hila, watang’olewa kutoka ndani yake.+

Maelezo ya Chini