2 Samweli 9:1-13

9  Na Daudi akasema: “Je, bado kuna yeyote aliyebaki wa nyumba ya Sauli, ili nimwonyeshe fadhili zenye upendo+ kwa ajili ya Yonathani?”+  Basi nyumba ya Sauli ilikuwa na mtumishi ambaye jina lake lilikuwa Siba.+ Kwa hiyo wakamwita, akaja kwa Daudi, ndipo mfalme akamwambia: “Je, wewe ni Siba?” naye akasema: “Mimi ni mtumishi wako.”  Na mfalme akaendelea kusema: “Je, hakuna kabisa mtu wa nyumba ya Sauli, ili nimwonyeshe fadhili zenye upendo za Mungu?”+ Hivyo Siba akamwambia mfalme: “Bado kuna mwana wa Yonathani, mwenye kulemaa miguu.”+  Kisha mfalme akamwambia: “Yuko wapi?” Kwa hiyo Siba akamwambia mfalme: “Tazama! Yuko katika nyumba ya Makiri+ mwana wa Amieli kule Lo-debari.”+  Mara moja Mfalme Daudi akatuma ujumbe kumchukua kutoka katika nyumba ya Makiri mwana wa Amieli kule Lo-debari.  Wakati Mefiboshethi mwana wa Yonathani mwana wa Sauli alipoingia kwa Daudi, akaanguka mara moja kifudifudi, akasujudu.+ Ndipo Daudi akasema: “Mefiboshethi!” naye akajibu: “Mimi hapa, mtumishi wako.”  Na Daudi akaendelea kumwambia: “Usiogope, kwa maana hakika nitakuonyesha fadhili zenye upendo+ kwa ajili ya Yonathani baba yako;+ nami nitakurudishia mashamba+ yote ya Sauli babu yako, nawe utakula mkate mezani pangu sikuzote.”+  Basi akasujudu na kusema: “Mtumishi wako ni nani, hata ukageuza uso wako kuelekea mbwa aliyekufa+ kama mimi?”  Sasa mfalme akamwita Siba, mtumishi wa Sauli, akamwambia: “Kila kitu ambacho kilikuwa cha Sauli na cha nyumba yake yote,+ nampa mjukuu wa bwana wako. 10  Nawe umlimie udongo, wewe na wana wako na watumishi wako, nawe utayakusanya mavuno, nayo yatakuwa chakula kwa walio wa mjukuu wa bwana wako, nao watakula; lakini Mefiboshethi, mjukuu wa bwana wako, atakula mkate mezani pangu sikuzote.”+ Basi Siba alikuwa na wana 15 na watumishi 20.+ 11  Kwa hiyo Siba akamwambia mfalme: “Mtumishi wako atafanya kulingana na yote ambayo mfalme bwana wangu anamwamuru mtumishi wake; lakini Mefiboshethi+ anakula mezani pangu kama mmoja wa wana wa mfalme.” 12  Mefiboshethi alikuwa na mwana mchanga ambaye jina lake lilikuwa Mika,+ na wote waliokuwa wakikaa katika nyumba ya Siba walikuwa watumishi wa Mefiboshethi. 13  Na Mefiboshethi alikuwa anakaa katika Yerusalemu, kwa maana alikuwa akila sikuzote mezani pa mfalme;+ naye alikuwa amelemaa miguu yote miwili.+

Maelezo ya Chini