2 Samweli 2:1-32

2  Na ikawa baadaye kwamba Daudi akamuuliza Yehova,+ akisema: “Je, nipande kwenda katika moja la majiji ya Yuda?” Ndipo Yehova akamwambia: “Panda uende.” Na Daudi akaendelea kusema: “Nipande kwenda wapi?” Ndipo akasema: “Hebroni.”+  Basi Daudi akaenda huko na wake zake wawili pia, Ahinoamu+ Myezreeli, na Abigaili+ mke wa Nabali Mkarmeli.  Na Daudi akawaleta wale watu+ waliokuwa pamoja naye, kila mmoja na nyumba yake; nao wakaanza kukaa katika majiji ya eneo la Hebroni.  Ndipo watu wa Yuda+ wakaja, wakamtia Daudi mafuta+ hapo awe mfalme juu ya nyumba ya Yuda.+ Nao wakaja kumwambia Daudi, wakisema: “Watu wa Yabesh-gileadi ndio waliomzika Sauli.”  Basi Daudi akatuma wajumbe kwa watu wa Yabesh-gileadi+ na kuwaambia: “Mbarikiwe na Yehova,+ kwa kuwa mmeonyesha hizi fadhili zenye upendo+ kwa bwana wenu, kwa Sauli, kwa maana mlimzika.+  Na sasa Yehova na awaonyeshe ninyi fadhili zenye upendo+ na uaminifu, nami pia nitawaonyesha wema huu kwa sababu mmefanya jambo hili.+  Na sasa mikono yenu na ijitie nguvu na muwe wanaume mashujaa,+ kwa sababu Sauli bwana wenu amekufa, na nyumba ya Yuda wamenitia mimi mafuta niwe mfalme+ juu yao.”  Lakini Abneri+ mwana wa Neri mkuu wa jeshi lililokuwa la Sauli, alimchukua Ish-boshethi,+ mwana wa Sauli, akamvusha mpaka Mahanaimu,+  akamfanya kuwa mfalme juu ya Gileadi+ na Waashuri na Yezreeli+ na juu ya Efraimu+ na Benyamini+ na juu ya Israeli yote. 10  Ish-boshethi, mwana wa Sauli, alikuwa na umri wa miaka 40 alipokuwa mfalme juu ya Israeli, naye akatawala akiwa mfalme kwa miaka miwili. Ni nyumba ya Yuda+ peke yao ndio waliomfuata Daudi. 11  Na hesabu ya siku ambazo Daudi alikuwa mfalme katika Hebroni juu ya nyumba ya Yuda ikawa miaka saba na miezi sita.+ 12  Baada ya muda Abneri mwana wa Neri na watumishi wa Ish-boshethi, mwana wa Sauli, wakatoka Mahanaimu+ kwenda Gibeoni.+ 13  Naye Yoabu+ mwana wa Seruya+ na watumishi wa Daudi wakaondoka na baadaye wakakutana pamoja kando ya kidimbwi cha Gibeoni; nao wakaendelea kuketi, hawa upande huu wa kile kidimbwi na wale upande ule wa kile kidimbwi. 14  Mwishowe Abneri akamwambia Yoabu: “Tafadhali, acha vijana wasimame, wapambane mbele yetu.” Naye Yoabu akasema: “Acha wasimame.” 15  Basi wakasimama, wakavuka kwa hesabu yao, kumi na wawili wa Benyamini na Ish-boshethi,+ mwana wa Sauli, na kumi na wawili kutoka kwa watumishi wa Daudi. 16  Ndipo wakaanza kukamatana kwa vichwa, huku upanga wa kila mmoja ukiwa katika ubavu wa mwenzake, nao wakaanguka pamoja. Na mahali hapo pakaitwa Helkath-hasurimu, napo ni katika Gibeoni.+ 17  Na mapigano yakawa magumu mno siku hiyo, na mwishowe Abneri+ pamoja na watu wa Israeli wakashindwa mbele ya watumishi wa Daudi. 18  Basi wale wana watatu wa Seruya+ walikuwa hapo, Yoabu+ na Abishai+ na Asaheli;+ na Asaheli alikuwa mwepesi kwa miguu yake, kama mmoja wa swala+ walio porini. 19  Na Asaheli akamfuatilia Abneri, naye hakwenda upande wa kuume wala wa kushoto, aache kumfuatilia Abneri. 20  Baada ya muda Abneri akatazama nyuma na kusema: “Je, ni wewe, Asaheli?” naye akasema: “Ni mimi.” 21  Ndipo Abneri akamwambia: “Geuka upande wako wa kuume au wa kushoto, umkamate mmoja wa vijana awe wako na uchukue kile utakachovua+ kutoka kwake kiwe chako.” Na Asaheli hakutaka kugeuka kando, aache kumfuatilia. 22  Kwa hiyo Abneri akamwambia tena Asaheli: “Geuza mwendo wako, acha kunifuatilia. Kwa nini nikupige ufe na kuanguka chini?+ Hapo, basi, ningewezaje kuinua uso wangu kumwelekea Yoabu ndugu yako?” 23  Lakini akaendelea kukataa kugeuka kando; ndipo Abneri akampiga tumboni+ kwa ncha ya nyuma ya mkuki, hata mkuki ukatokea upande wake wa nyuma; akaanguka hapo, akafa papo hapo. Na ikawa kwamba watu wote waliofika mahali ambapo Asaheli alianguka kisha akafa wakawa wakisimama tuli.+ 24  Na Yoabu na Abishai wakamfuatilia Abneri. Na jua lilipokuwa likitua wakafika katika kilima cha Ama, kilicho mbele ya Gia kwenye njia ya nyika ya Gibeoni.+ 25  Ndipo wana wa Benyamini wakakusanyika nyuma ya Abneri, wakawa kundi moja, wakaendelea kusimama juu ya kilima kimoja. 26  Kisha Abneri akamwita Yoabu na kusema: “Je, upanga utakula+ bila kukoma? Je, hujui hakika kwamba uchungu ndio utakaotokea mwishowe?+ Basi, itachukua muda gani kabla hujawaambia watu warudi nyuma, waache kuwafuatilia ndugu zao?”+ 27  Naye Yoabu akasema: “Kama Mungu wa kweli anavyoishi,+ kama usingalisema,+ ni wakati wa asubuhi tu ndipo watu wangaliondolewa, kila mmoja aache kumfuatilia ndugu yake.” 28  Basi Yoabu akapiga baragumu,+ kisha watu wote wakasimama, wakaacha kuwafuatilia Israeli, wala hawakurudi tena kupigana upya. 29  Naye Abneri na watu wake wakapiga mwendo kupitia Araba+ usiku huo wote, wakavuka Yordani,+ wakapiga mwendo kuupitia mtaro mzima, mwishowe wakafika Mahanaimu.+ 30  Naye Yoabu akageuka, akaacha kumfuatilia Abneri, akaanza kuwakusanya watu wote pamoja. Na watumishi wa Daudi walipungukiwa na watu kumi na tisa pamoja na Asaheli. 31  Na watumishi wa Daudi walikuwa wamepiga watu wa Benyamini na wa Abneri—walikuwa watu 360 waliokufa.+ 32  Nao wakamchukua Asaheli,+ wakamzika katika kaburi la baba yake,+ katika Bethlehemu.+ Kisha Yoabu na watu wake wakapiga mwendo usiku kucha, na nuru ikawapambazukia Hebroni.+

Maelezo ya Chini