Mathayo 11:1-30

11  Basi Yesu alipokuwa amemaliza kuwapa maagizo wanafunzi wake kumi na wawili, aliondoka akafundishe na kuhubiri katika majiji yao.+  Lakini Yohana, akiwa amekwisha kusikia katika jela+ juu ya kazi za Kristo, akawatuma wanafunzi wake mwenyewe  na kumwambia: “Je, wewe ndiye Yule Anayekuja, au tumtarajie mwingine?”+  Yesu akajibu, akawaambia: “Nendeni mkamwambie Yohana mambo mnayosikia na kuona:  Vipofu wanaona tena,+ vilema+ wanatembea, wenye ukoma+ wanatakaswa na viziwi+ wanasikia, wafu+ wanafufuliwa, maskini wanatangaziwa habari njema;+  na mwenye furaha ni yule asiyepata ndani yangu sababu ya kukwazika.”+  Hao walipokuwa wameondoka na kwenda, Yesu akaanza kuuambia umati habari ya Yohana: “Mlienda nyikani kuona nini?+ Tete likitikiswa na upepo?+  Basi, mlienda kuona nini? Mtu aliyevaa mavazi mororo? Kwani, wale wanaovaa mavazi mororo wamo katika nyumba za wafalme.+  Basi, kwa kweli kwa nini mlitoka kwenda? Kuona nabii? Ndiyo, nawaambia ninyi, na ni zaidi ya nabii.+ 10  Huyu ndiye ambaye imeandikwa hivi kumhusu, ‘Tazama! Mimi mwenyewe ninamtuma mjumbe wangu mbele ya uso wako, ambaye atatayarisha njia yako mbele yako!’+ 11  Kwa kweli nawaambia ninyi, Kati ya wale waliozaliwa na wanawake+ hajatokea mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; lakini mtu aliye mdogo zaidi katika ufalme+ wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye. 12  Lakini tangu siku za Yohana Mbatizaji mpaka sasa ufalme wa mbinguni ndio mradi ambao watu wanajikaza kuufikia, na wale wanaojikaza wanaufikia.+ 13  Kwa maana wote, Manabii na Sheria, walitoa unabii mpaka kufikia Yohana;+ 14  nanyi mkitaka kukubali hili, Yeye mwenyewe ndiye ‘Eliya ambaye anakusudiwa kuja.’+ 15  Yule aliye na masikio na asikilize.+ 16  “Nitakilinganisha kizazi hiki na nani?+ Ni kama watoto wachanga ambao wameketi masokoni wanaowapaazia sauti wachezaji wenzao,+ 17  wakisema, ‘Tuliwapigia ninyi filimbi, lakini hamkucheza dansi; tulitoa sauti za kuomboleza, lakini hamkujipiga-piga kwa huzuni.’+ 18  Kulingana na hilo, Yohana alikuja akiwa hali chakula wala kunywa,+ na bado watu wanasema, ‘Ana roho mwovu’; 19  Mwana wa binadamu alikuja akiwa anakula na kunywa,+ na bado watu wanasema, ‘Tazama! Mtu mlafi na mwenye mazoea ya kunywa divai, rafiki ya wakusanya-kodi na watenda-dhambi.’+ Hata hivyo, hekima huonyeshwa kuwa yenye uadilifu kwa matendo yake.”+ 20  Ndipo akaanza kuyashutumu majiji ambamo nyingi za kazi zake zenye nguvu zilikuwa zimetendeka, kwa sababu hayakutubu:+ 21  “Ole wako, Korazini! Ole wako, Bethsaida!+ kwa sababu kama zile kazi zenye nguvu zingalifanyika katika Tiro na Sidoni ambazo zilifanyika ndani yenu, wangalitubu zamani za kale katika nguo ya gunia na majivu.+ 22  Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi, Itakuwa rahisi zaidi kwa Tiro na Sidoni katika Siku ya Hukumu+ kuliko kwenu.+ 23  Na wewe, Kapernaumu,+ je, labda utainuliwa mpaka mbinguni? Utashuka+ chini mpaka katika Kaburi;*+ kwa sababu kama zile kazi zenye nguvu zilizofanyika ndani yako zingalifanyika Sodoma, lingalidumu mpaka leo hii. 24  Kwa sababu hiyo ninawaambia ninyi, Itakuwa rahisi zaidi kwa nchi ya Sodoma katika Siku ya Hukumu kuliko kwenu.”+ 25  Wakati huo Yesu akajibu, akasema: “Ninakusifu wewe hadharani, Baba, Bwana wa mbingu na dunia, kwa sababu umewaficha mambo haya wenye hekima na wenye akili na umeyafunua kwa watoto.+ 26  Ndiyo, Ee Baba, kwa sababu kufanya hivyo kulikuwa ndiyo njia iliyokubaliwa nawe. 27  Baba yangu amenipa mimi vitu vyote,+ na hakuna yeyote anayemjua Mwana kabisa ila Baba,+ wala yeyote hamjui Baba kabisa ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana anapenda kumfunulia.+ 28  Njooni kwangu, nyote mnaotaabika na kulemewa na mizigo,+ nami nitawaburudisha ninyi. 29  Chukueni nira+ yangu na mjifunze kutoka kwangu,+ kwa maana mimi ni mwenye tabia-pole+ na mnyenyekevu moyoni, nanyi mtapata burudisho+ kwa ajili ya nafsi zenu. 30  Kwa maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni mwepesi.”+

Maelezo ya Chini

Hadesi. Tazama Nyongeza 4.