Hamia kwenye habari

Ndugu Kenneth Cook akionyesha toleo lililochapishwa la Tafsiri ya Ulimwengu Mpya katika lugha ya Twi

MACHI 9, 2021
GHANA

Mashahidi wa Yehova Watoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya Iliyorekebishwa Katika Lugha ya Twi (Akuapem)

Mashahidi wa Yehova Watoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya Iliyorekebishwa Katika Lugha ya Twi (Akuapem)

Machi 7, 2021, Mashahidi wa Yehova walitoa Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliyorekebishwa katika lugha ya Twi (Akuapem). Ndugu Kenneth Cook, mshiriki wa Baraza Linaloongoza alitoa Biblia hiyo katika programu iliyorekodiwa mapema. Biblia hiyo ilipatikana katika mfumo wa kidijitali baada ya programu.

Tukio hilo lilipeperushwa kwenye televisheni kupitia satelaiti. Wahubiri walio katika maeneo ya mbali walisikiliza pia kupitia simu. Kwa njia hiyo, idadi kubwa ya wahubiri 98,000 wanaozungumza lugha ya Twi walifaulu kufurahia programu hiyo. Lugha ya Twi inazungumzwa na watu wengi nchini Ghana. Ingawa kuna lahaja nyingi za Kitwi, watu wengi zaidi wanaelewa Kitwi cha Akuapem. Mradi wa kutafsiri Biblia hiyo ulifanywa na watafsiri sita na ilichukua miaka mitatu na nusu kukamilisha.

Mtafsiri mmoja alisema hivi: “Yehova alituwezesha kutimiza mgawo huu muhimu sana. Sasa ninasadiki zaidi kwamba Mungu amezimia kufanya Neno lake lipatikane kwa watu wengi kadiri iwezekanavyo.”

Tunashangilia pamoja na ndugu zetu wanaozungumza lugha ya Twi kwa sababu ya kutolewa kwa Biblia hii. Katika nyakati hizi ngumu, tuna uhakika kwamba Neno la Mungu litatupa nguvu na hekima.—Zaburi 19:7.