KĨTHOOMO GĨA KWIRITANA GĨA 18
RWĨMBO 65 Songa Mbele!
Atana ba Baaba Babeethĩ—Igerekanieni na Timotheo na Mariko
“Ujukie Mariko bwijanie nawe; tontu nowe mwega ningi nantethagia ngugine iria nditaga.”—2 TIM. 4:11.
JAMBO KUU
Jinsi mfano wa Marko na Timotheo unavyoweza kuwasaidia ndugu vijana kusitawisha sifa wanazohitaji ili kuwatumikia wengine kikamili zaidi.
1-2. Nĩ mantũ jarĩkũ jamoomũ jarĩngĩrigĩĩria Timotheo na Mariko kwiritanĩria gũtumĩkĩra bangĩ nkũrũki?
NDUGU vijana, je, mngependa kutimiza mengi zaidi katika utumishi wa Yehova na kuwasaidia zaidi ndugu na dada katika kutaniko lenu? Bila shaka mngependa kufanya hivyo. Inafurahisha sana kuona vijana wengi wanaowatumikia wengine kwa hiari! (Zab. 110:3) Hata hivyo, huenda ukakabili changamoto. Je, unasita kupanua huduma yako kwa sababu hujui mambo yatakayotukia wakati ujao? Je, umewahi kusita kukubali mgawo kwa sababu ulihisi kwamba huwezi kuutimiza vizuri? Ikiwa ndivyo, wewe si wa kwanza kuhisi hivyo.
2 Marko na Timotheo walikabili changamoto kama hizo. Lakini hawakuruhusu kutokujua mambo yatakayotukia wakati ujao au kutokuwa na uzoefu kuwazuie kuwatumikia wengine. Inaelekea kwamba Marko alikuwa akiishi maisha yenye kustarehesha nyumbani pamoja na mama yake, wakati mtume Paulo na Barnaba walipomwalika aandamane nao katika safari yao ya kwanza ya umishonari. (Mdo. 12:12, 13, 25) Marko aliacha mazingira aliyozoea ili kupanua huduma yake. Kwanza, alihamia Antiokia. Kisha, aliambatana na Paulo na Barnaba katika maeneo mengine ya mbali. (Mdo. 13:1-5) Vivyo hivyo, inaelekea Timotheo alikuwa akiishi na wazazi wake Paulo alipomwalika ajiunge naye katika kazi ya kuhubiri. Akiwa kijana asiye na uzoefu, Timotheo angeweza kuhisi kwamba hawezi kutimiza vizuri mgawo huo. (Linganisha 1 Wakorintho 16:10, 11 na 1 Timotheo 4:12.) Hata hivyo, alikubali mwaliko wa Paulo na matokeo ni kwamba alifurahia baraka nyingi sana.—Mdo. 16:3-5.
3. (a) Nĩmbi bikwonania Paũlũ noonaga Timotheo na Mariko barĩ ba gĩtũmi? (2 Timotheo 4:6, 9, 11) (Tega kinya mbica.) (b) Nĩ biũria birĩkũ tũkaarĩĩria kĩthoomone gĩkĩ?
3 Marko na Timotheo walipata uzoefu wenye thamani na walijifunza kubeba majukumu mazito wakiwa vijana. Paulo aliwathamini sana vijana hao hivi kwamba baadaye alipokuwa karibu kuuawa aliwaomba waende kumwona. (Soma 2 Timotheo 4:6, 9, 11.) Ni sifa gani nzuri ambazo Marko na Timotheo walikuwa nazo zilizomfanya Paulo awapende? Ndugu vijana wanawezaje kuiga mtazamo wao? Na wanaume vijana wanaweza kunufaikaje na ushauri wa Paulo wenye upendo?
Marko na Timotheo walipendwa na Paulo kwa sababu walibeba majukumu mazito wakiwa wangali vijana (Tazama fungu la 3) b
ĨTHĨRWA NA WENDI BWA GŨTŨMĨKĨRA BANGĨ TA MARIKO
4-5. Nĩatĩa Mariko oonanĩrie naarĩ na wendi bwa gũtumĩkĩra bangĩ?
4 Kulingana na kitabu kimoja cha marejeo, kuwatumikia au kuwahudumia wengine kunamaanisha kuchukua hatua ya kwanza kuwasaidia “kwa bidii na bila kuacha.” Marko aliweka kielelezo kizuri kuhusiana na hilo. Huenda Marko alivunjika moyo, Paulo alipokataa kwenda pamoja naye katika safari yake ya pili ya umishonari. (Mdo. 15:37, 38) Lakini hakuruhusu jambo hilo limzuie kuwatumikia ndugu na dada zake.
5 Marko alikubali mgawo wa utumishi na kwenda pamoja na Barnaba, binamu yake. Miaka 11 hivi baadaye, Marko alikuwa miongoni mwa watu waliomtegemeza Paulo alipofungwa gerezani kwa mara ya kwanza huko Roma. (Flm. 23, 24) Kwa kweli, Paulo alithamini sana msaada huo hivi kwamba alimfafanua Marko kuwa “chanzo cha faraja nyingi.”—Kol. 4:10, 11.
6. Nĩatĩa Mariko aagunĩkĩre tontũ bwa gũtuma ũcoore na antũ bagimaru gĩkĩrundu? (Tega nteto irĩa irĩ gaiti.)
6 Marko alinufaika kwa kushirikiana kwa ukaribu na Wakristo wakomavu. Baada ya kuwa pamoja na Paulo kwa muda fulani jijini Roma, Marko alijiunga na mtume Petro katika jiji la Babiloni. Walisitawisha uhusiano wa karibu sana hivi kwamba Petro alimwita “Marko, mwanangu.” (1 Pet. 5:13) Walipokuwa wakifanya kazi pamoja, huenda Petro alimsimulia rafiki yake kijana habari nyingi hususa kuhusu maisha na huduma ya Yesu ambazo baadaye Marko aliziandika katika Injili yake. a
7. Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ ũrĩa ũgĩtwa Seung-Woo aaigerekanĩrie na Mariko? (Tega kinya mbica.)
7 Marko alikuwa na mengi ya kufanya katika utumishi wake na aliendelea kushirikiana kwa ukaribu pamoja na ndugu wakomavu. Unawezaje kumwiga Marko? Ikiwa hujapata pendeleo fulani la utumishi, uwe na subira na uendelee kutafuta njia nyingine za kumtumikia Yehova na kutaniko lako. Fikiria mfano wa Seung-Woo, ambaye sasa anatumikia akiwa mzee. Alipokuwa kijana, alijilinganisha na ndugu wengine vijana. Baadhi yao walipewa mapendeleo kabla yake. Seung-Woo alihisi amepuuzwa na hatimaye aliwaeleza ndugu wakomavu jambo hilo. Mzee mmoja wa kutaniko alimpendekezea kwamba afanye yote awezayo kuwatumikia wengine hata kama mara nyingine matendo hayo mazuri hayaonwi na watu wengine. Ushauri huo ulimchochea Seung-Woo ajitolee kuwasaidia ndugu na dada wenye umri mkubwa waliokuwa wanahitaji usafiri ili waweze kuhudhuria mikutano. Anakumbuka hivi: “Nilijifunza kinachomaanishwa na kuwatumikia wengine kikamili zaidi. Nilipata shangwe inayotokana na kuwasaidia wengine kwa njia hususa.”
Ndugu vijana wananufaikaje kwa kushirikiana kwa ukawaida na ndugu wakomavu? (Tazama fungu la 7)
ONANIA NŨKŨMAKĨRA BANGĨ KAMMA TA TIMOTHEO
8. Nĩkĩ Paũlũ aathuurĩre Timotheo nĩkenda betania nawe? (Afilipi 2:19-22)
8 Paulo alihitaji waandamani wenye ujasiri aliporudi katika majiji ambayo awali alikabili upinzani. Kwanza, alimchagua Mkristo mzoefu aliyeitwa Sila aandamane naye. (Mdo. 15:22, 40) Baadaye, Paulo alimchagua pia Timotheo ajiunge naye. Kwa nini Paulo alimchagua Timotheo? Jambo moja ni kwamba alishuhudiwa vema na akina ndugu. (Mdo. 16:1, 2) Pia, aliwajali watu kwa unyoofu.—Soma Wafilipi 2:19-22.
9. Nĩatĩa Timotheo oonanĩrie kamma naamakagĩra atana na aarĩ ba baaba?
9 Tangu alipoanza huduma yake pamoja na Paulo, Timotheo alionyesha kwamba alitanguliza mahitaji ya wengine kuliko mahitaji yake. Kwa sababu hiyo, Paulo hakuwa na wasiwasi alipomwacha Beroya ili awatie moyo wanafunzi wapya huko. (Mdo. 17:13, 14) Katika pindi hiyo, bila shaka Timotheo alinufaika na kielelezo cha Sila, ambaye pia alibaki Beroya. Hata hivyo, baadaye Paulo alimtuma Timotheo akiwa peke yake ili akawatie nguvu Wakristo katika jiji la Thesalonike. (1 The. 3:2, maelezo ya chini) Katika kipindi cha miaka 15 hivi iliyofuata, Timotheo alijifunza ‘kulia na wale wanaolia,’ na kuonyesha hisia mwenzi kwa yeyote aliyekuwa akiteseka. (Rom. 12:15; 2 Tim. 1:4) Wanaume Wakristo vijana wanawezaje kumwiga Timotheo?
10. Nĩatĩa mũtana wa baaba Woo Jae aairitanĩre kũmakĩra bangĩ?
10 Ndugu anayeitwa Woo Jae alijifunza kuwaonyesha zaidi wengine upendezi wa kibinafsi. Alipokuwa kijana, ilikuwa vigumu kwa Woo Jae kuwa na mazungumzo pamoja na ndugu na dada wenye umri mkubwa. Hivyo, angewasalimu tu katika Jumba la Ufalme na kuondoka. Mzee wa kutaniko alimpendekezea Woo Jae aanzishe mazungumzo kwa kuwaambia ndugu na dada zake mambo aliyothamini kuwahusu. Mzee huyo alimhimiza pia afikirie mambo ambayo huenda wengine wanapendezwa nayo. Woo Jae alitumia ushauri huo alipokuwa akizungumza na wengine. Woo Jae, ambaye leo ni mzee wa kutaniko, anasema hivi: “Sasa ni rahisi zaidi kwangu kuwa na mazungumzo yenye kujenga pamoja na watu wenye umri tofauti. Ninafurahi kwamba sasa ninaelewa vizuri zaidi mahangaiko ya watu wengine. Jambo hilo limeniwezesha kuwasaidia vizuri zaidi waabudu wenzangu.”
11. Nĩatĩa atana ba baaba babeethĩ bomba kwonania kamma nĩbakũmakĩra bangĩ kĩũthũranone? (Tega kinya mbica.)
11 Enyi ndugu vijana, mnaweza pia kujifunza kuwaonyesha wengine upendezi wa kibinafsi. Unapokuwa katika mikutano, waonyeshe watu wenye umri na malezi mbalimbali upendezi wa kibinafsi. Waulize kuhusu hali yao, na uwasikilize wanapojibu. Hilo litakusaidia kujua jinsi ya kuwasaidia. Labda utatambua kwamba wenzi wa ndoa wenye umri mkubwa wanahitaji kuonyeshwa jinsi ya kutumia JW Library®. Au huenda ukatambua kwamba hawana mwandamani wa kuhubiri pamoja nao. Je, unaweza kuwasaidia kwa kuwaonyesha jinsi ya kutumia vifaa vyao vya kielektroni au kufanya mipango ya kuhubiri pamoja nao? Kwa kuchukua hatua ya kwanza ili kuwasaidia wengine, utawawekea mfano mzuri wengine kutanikoni.
Akina ndugu vijana wanaweza kulisaidia kutaniko kwa njia nyingi hususa (Tazama fungu la 11)
GUNĨKA KUUMANIA NA ŨTAARO BWA WENDO BWA PAŨLŨ
12. Nĩatĩa antũ arũme babeethĩ bomba kũgunĩka kuumania na ũtaaro bwa Paũlũ kĩrĩ Timotheo?
12 Paulo alimpatia Timotheo ushauri unaofaa ili afanikiwe maishani na katika huduma yake. (1 Tim. 1:18; 2 Tim. 4:5) Ninyi ndugu vijana mnaweza pia kunufaika na ushauri wenye upendo wa Paulo. Jinsi gani? Soma barua mbili za Paulo kwa Timotheo kana kwamba zimeandikwa kwa ajili yako, na uone ni ushauri gani unaoweza kuutumia maishani mwako. Fikiria mifano michache ifuatayo.
13. Nĩmbi tũkũbatara nĩkenda twĩthĩrwa na ngwatanĩro ya akuĩ amwe na Mũrungu?
13 “Endelea kujizoeza ukiwa na lengo la ujitoaji-kimungu.” (1 Tim. 4:7b) Ujitoaji-kimungu ni nini? Ni kushikamana kabisa na Yehova na kutamani kufanya mambo yanayomfurahisha. Kwa kuwa hatuzaliwi tukiwa na sifa hiyo, tunahitaji kuisitawisha. Jinsi gani? Neno la Kigiriki linalotafsiriwa “endelea kujizoeza” mara nyingi lilitumiwa kufafanua mazoezi makali ambayo wanamichezo walifanya ili kujitayarisha kwa ajili ya shindano. Wanamichezo hao walihitaji kujitia nidhamu. Sisi pia tunahitaji kujitia nidhamu ili tusitawishe mazoea ambayo yatatusaidia tumkaribie zaidi Yehova.
14. Nĩ mworoto jũrĩkũ tũbuĩrĩte kwĩthĩrwa tũrĩ naju rĩrĩa tũkũthooma Bibiria? Ejana ngerekano.
14 Unapositawisha zoea la kusoma Biblia, kumbuka kwamba lengo lako ni kumkaribia zaidi Yehova. Kwa mfano, unaweza kujifunza nini kuhusu mazungumzo kati ya Yesu na yule mtawala kijana aliyekuwa tajiri? (Marko 10:17-22) Kijana huyo aliamini kwamba Yesu alikuwa Masihi, lakini hakuwa na imani ya kutosha kuwa mfuasi wake. Hata hivyo, Yesu ‘alimpenda.’ Je, huguswi moyo na jinsi Yesu alivyozungumza na mwanamume huyo kijana? Bila shaka, Yesu alitaka kijana huyo afanye uamuzi wenye hekima. Yesu alikuwa pia akionyesha upendo wa Yehova kwa kijana huyo. (Yoh. 14:9) Unapotafakari simulizi hilo na hali zako, jiulize hivi, ‘Ninahitaji kufanya nini ili nimkaribie zaidi Yehova na kuwatumikia wengine kikamili zaidi?’
15. Nĩkĩ mũtana wa baaba ũmwĩthĩ abuĩrĩte gwĩka ngerekano ĩnjega? Taarĩĩria. (1 Timotheo 4:12, 13)
15 “Uwe mfano mzuri kwa waaminifu.” (Soma 1 Timotheo 4:12, 13.) Paulo alimhimiza Timotheo asitawishe ustadi wa kusoma na kufundisha, lakini pia asitawishe sifa kama vile upendo, imani, na usafi wa kiadili. Kwa nini? Kwa sababu mfano mzuri una nguvu kuliko maneno ambayo mtu anasema. Tuseme umepewa mgawo wa kutoa hotuba kuhusu jinsi tunavyoweza kuongeza bidii yetu katika huduma. Utakuwa na uhuru zaidi wa kutoa hotuba hiyo ikiwa unajitahidi kufanya yote unayoweza katika huduma yako. Mfano wako utaongezea nguvu maneno yako.—1 Tim. 3:13.
16. (a) Nĩ mantũ jarĩkũ jatano mũtana wa baaba ũmwĩthĩ abuĩrĩte kũthithia nĩkenda ethĩrwa arĩ ngerekano ĩnjega kĩrĩ bangĩ? (b) Nĩatĩa mũtana wa baaba ũmwĩthĩ oomba kwĩthĩrwa arĩ ngerekano ĩnjega kĩrĩ ‘nteto irĩa aragia’?
16 Kama inavyoonyeshwa katika 1 Timotheo 4:12, Paulo anataja mambo matano ambayo ndugu kijana anaweza kufanya ili awawekee wengine mfano mzuri. Unaweza kupanga kujifunza mambo hayo katika funzo lako la kibinafsi. Kwa mfano, tuseme unataka kuwa mfano mzuri zaidi “katika kusema.” Fikiria njia ambazo unaweza kutumia usemi wako kuwajenga wengine. Ikiwa bado unaishi nyumbani pamoja na wazazi wako, je, unaweza kuwaeleza mara nyingi zaidi kwamba unathamini mambo ambayo wanakufanyia? Baada ya mikutano, je, unaweza kumweleza ndugu au dada aliyekuwa na mgawo jambo ambalo ulithamini kuhusu sehemu yake? Unaweza pia kutoa maelezo kwa maneno yako mwenyewe mkutanoni. Jitihada zako za kuwa mfano mzuri katika kusema zitaonyesha kwamba unafanya maendeleo ya kiroho.—1 Tim. 4:15.
17. Nĩmbi biũmba gũtethia mũtana wa baaba ũmwĩthĩ gũkinyĩra mĩoroto yaawe ya gĩkĩrundu? (2 Timotheo 2:22)
17 “Zikimbie tamaa za ujana, lakini fuatilia uadilifu.” (Soma 2 Timotheo 2:22.) Paulo alimhimiza Timotheo ajilinde dhidi ya tamaa ambazo zingemkengeusha asifikie malengo yake ya kiroho na kuharibu uhusiano wake na Yehova. Huenda ukagundua kwamba utendaji fulani, ingawa si mbaya, unaweza kufanya ukose muda wa kutosha wa kufanya mambo ya kiroho. Kwa mfano, fikiria muda unaotumia katika michezo, kutumia intaneti, au katika michezo ya video. Je, unaweza kutumia sehemu ya muda huo kufanya mambo ya kiroho? Huenda unaweza kujitolea kusaidia kudumisha Jumba lenu la Ufalme au kuunga mkono mipango ya utumishi wa kigari. Ikiwa utashiriki katika utendaji kama huo, huenda ukapata marafiki wapya watakaokusaidia kuweka na kufikia malengo ya kiroho.
KWIRITANĨRIA GŨTUMĨKĨRA BANGĨ NĨKŨRETAGA ITHARIMO
18. Nĩkĩ tũũmba kuuga Timotheo na Mariko nĩbaairitanĩrĩtie, na nĩbaarĩ na ũtũũro bũrĩna kũgwĩrua?
18 Marko na Timotheo walijidhabihu ili kuwatumikia wengine kikamili zaidi, na walikuwa na maisha yenye kuridhisha na yaliyokuwa na utendaji mwingi. (Mdo. 20:35) Ili awatumikie waabudu wenzake, Marko alisafiri kwenda maeneo mengi ya mbali. Pia, aliandika simulizi lenye kusisimua la maisha na huduma ya Yesu. Timotheo alimsaidia Paulo kuanzisha makutaniko na kuwajenga akina ndugu na dada. Ni wazi kwamba Yehova alifurahishwa na roho ya kujidhabihu ambayo Marko na Timotheo walionyesha.
19. Nĩkĩ atana ba baaba babeethĩ babuĩrĩte gũtumĩra ũtaaro bwa Paũlũ kĩrĩ Timotheo, na maumĩĩra jakethĩrwa jarĩ jarĩkũ?
19 Upendo wa Paulo kwa Timotheo unaweza kuonekana wazi katika barua alizomwandikia rafiki yake huyo kijana. Barua hizo zilizoongozwa na roho takatifu zinaonyesha kwamba Yehova anawapenda sana ninyi wanaume vijana. Anataka mfanikiwe. Hivyo, fanya yote unayoweza ili kutumia ushauri wa Paulo wenye upendo na usitawishe tamaa ya kuwatumikia wengine kikamili zaidi. Ukifanya hivyo, utafurahia maisha yenye kuridhisha sasa na ‘utaushika imara uzima ulio wa kweli’ unaokuja.—1 Tim. 6:18, 19.
RWĨMBO 80 “Onjeni Mwone Kwamba Yehova Ni Mwema”
a Kwa kuwa alikuwa mwanamume mwenye hisia nyingi, Petro angeweza kumsimulia Marko kwa kina jinsi ambavyo Yesu alihisi na kutenda katika hali mbalimbali. Huenda hilo likatusaidia kuelewa kwa nini katika simulizi lake la maisha ya Yesu, mara nyingi Marko alifafanua hisia na matendo ya Yesu.—Marko 3:5; 7:34; 8:12.
b MAELEZO YA PICHA: Marko akishughulikia mahitaji ya Paulo na Barnaba katika safari yao ya umishonari. Kwa hiari, Timotheo analitembelea kutaniko ili kuliimarisha na kuwatia moyo akina ndugu.