Methali 10:1-32

10  Methali za Sulemani.+ Mwana mwenye hekima ndiye anayemfanya baba ashangilie,+ naye mwana mjinga ni huzuni ya mama yake.+  Hazina za mwovu hazitakuwa na faida,+ lakini uadilifu ndio utakaokomboa kutoka katika kifo.+  Yehova hataiacha nafsi ya mwadilifu iteswe na njaa,+ lakini atasukumia mbali tamaa ya waovu.+  Anayefanya kazi kwa mkono mlegevu atakuwa maskini,+ lakini mkono wa mwenye bidii ndio utakaomtajirisha.+  Mwana anayetenda kwa ufahamu anakusanya wakati wa kiangazi; mwana anayetenda kwa aibu analala usingizi mzito wakati wa mavuno.+  Baraka humkalia mwadilifu kichwani,+ lakini kinywa cha waovu, hufunika jeuri.+  Kumbukumbu la mwadilifu litabarikiwa,+ lakini jina la waovu litaoza.+  Mwenye hekima moyoni atazikubali amri,+ lakini mwenye midomo ya upumbavu atakanyagiwa chini.+  Anayetembea kwa utimilifu atatembea salama,+ lakini anayepotoa njia zake atajifanya mwenyewe ajulikane.+ 10  Anayekonyeza jicho lake atatokeza maumivu,+ na mwenye midomo ya upumbavu atakanyagiwa chini.+ 11  Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uzima;+ lakini kinywa cha waovu, hufunika jeuri.+ 12  Chuki huchochea ugomvi,+ lakini upendo hufunika hata makosa yote.+ 13  Hekima hupatikana kwenye midomo ya mtu mwenye uelewaji,+ lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa mtu ambaye amepungukiwa moyoni.+ 14  Wenye hekima ndio wanaoweka hazina ya ujuzi,+ lakini kinywa cha mpumbavu kinakaribia uharibifu wenyewe.+ 15  Vitu vyenye thamani vya tajiri ni mji wake wenye nguvu.+ Uharibifu wa watu wa hali ya chini ni umaskini wao.+ 16  Utendaji wa mwadilifu hutokeza uzima;+ mazao ya mwovu hutokeza dhambi.+ 17  Anayeshika nidhamu ni njia ya uzima,+ lakini anayeacha karipio anasababisha kupotea.+ 18  Mtu anayefunika chuki ana midomo ya uwongo,+ naye anayeleta habari mbaya ni mjinga.+ 19  Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na kosa,+ lakini anayezuia midomo yake anatenda kwa busara.+ 20  Ulimi wa mwadilifu ni fedha bora,+ moyo wa mwovu una thamani ndogo.+ 21  Midomo ya mwadilifu huendelea kulisha wengi,+ lakini wapumbavu huendelea kufa kwa sababu ya kupungukiwa moyoni.+ 22  Baraka ya Yehova—hiyo ndiyo hutajirisha,+ naye haongezi maumivu pamoja nayo.+ 23  Kwa mtu mjinga kuendeleza mwenendo mpotovu ni kama mchezo,+ lakini mtu mwenye utambuzi ana hekima.+ 24  Kitu chenye kumwogopesha mwovu—hicho ndicho kitakachompata;+ lakini tamaa ya mwadilifu itatimizwa.+ 25  Kama wakati upepo wa dhoruba unapopita, ndivyo na mwovu asivyokuwapo tena;+ lakini mwadilifu ni msingi mpaka wakati usio na kipimo.+ 26  Kama siki kwenye meno na kama moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mtu mvivu kwa wale wanaomtuma.+ 27  Kumwogopa Yehova kutaongeza siku,+ lakini miaka ya waovu itafupishwa.+ 28  Tarajio la waadilifu ni kushangilia,+ lakini tumaini lenyewe la waovu litapotea.+ 29  Njia ya Yehova ni ngome kwa mtu asiye na lawama,+ lakini wale wanaozoea kutenda mambo yenye kuumiza wataharibiwa.+ 30  Naye mwadilifu, mpaka wakati usio na kipimo hatafanywa apepesuke,+ lakini waovu, hawataendelea kukaa duniani.+ 31  Kinywa cha mwadilifu—hicho huzaa tunda la hekima,+ lakini ulimi wa upotovu utakatiliwa mbali.+ 32  Midomo ya mwadilifu​​—​hiyo hujua nia njema,+ lakini kinywa cha waovu ni upotovu.+

Maelezo ya Chini