Methali 10:1-32
10 Methali za Sulemani.+
Mwana mwenye hekima ndiye anayemfanya baba ashangilie,+ naye mwana mjinga ni huzuni ya mama yake.+
2 Hazina za mwovu hazitakuwa na faida,+ lakini uadilifu ndio utakaokomboa kutoka katika kifo.+
3 Yehova hataiacha nafsi ya mwadilifu iteswe na njaa,+ lakini atasukumia mbali tamaa ya waovu.+
4 Anayefanya kazi kwa mkono mlegevu atakuwa maskini,+ lakini mkono wa mwenye bidii ndio utakaomtajirisha.+
5 Mwana anayetenda kwa ufahamu anakusanya wakati wa kiangazi; mwana anayetenda kwa aibu analala usingizi mzito wakati wa mavuno.+
6 Baraka humkalia mwadilifu kichwani,+ lakini kinywa cha waovu, hufunika jeuri.+
7 Kumbukumbu la mwadilifu litabarikiwa,+ lakini jina la waovu litaoza.+
8 Mwenye hekima moyoni atazikubali amri,+ lakini mwenye midomo ya upumbavu atakanyagiwa chini.+
9 Anayetembea kwa utimilifu atatembea salama,+ lakini anayepotoa njia zake atajifanya mwenyewe ajulikane.+
10 Anayekonyeza jicho lake atatokeza maumivu,+ na mwenye midomo ya upumbavu atakanyagiwa chini.+
11 Kinywa cha mwadilifu ni chemchemi ya uzima;+ lakini kinywa cha waovu, hufunika jeuri.+
12 Chuki huchochea ugomvi,+ lakini upendo hufunika hata makosa yote.+
13 Hekima hupatikana kwenye midomo ya mtu mwenye uelewaji,+ lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa mtu ambaye amepungukiwa moyoni.+
14 Wenye hekima ndio wanaoweka hazina ya ujuzi,+ lakini kinywa cha mpumbavu kinakaribia uharibifu wenyewe.+
15 Vitu vyenye thamani vya tajiri ni mji wake wenye nguvu.+ Uharibifu wa watu wa hali ya chini ni umaskini wao.+
16 Utendaji wa mwadilifu hutokeza uzima;+ mazao ya mwovu hutokeza dhambi.+
17 Anayeshika nidhamu ni njia ya uzima,+ lakini anayeacha karipio anasababisha kupotea.+
18 Mtu anayefunika chuki ana midomo ya uwongo,+ naye anayeleta habari mbaya ni mjinga.+
19 Katika wingi wa maneno hapakosi kuwa na kosa,+ lakini anayezuia midomo yake anatenda kwa busara.+
20 Ulimi wa mwadilifu ni fedha bora,+ moyo wa mwovu una thamani ndogo.+
21 Midomo ya mwadilifu huendelea kulisha wengi,+ lakini wapumbavu huendelea kufa kwa sababu ya kupungukiwa moyoni.+
22 Baraka ya Yehova—hiyo ndiyo hutajirisha,+ naye haongezi maumivu pamoja nayo.+
23 Kwa mtu mjinga kuendeleza mwenendo mpotovu ni kama mchezo,+ lakini mtu mwenye utambuzi ana hekima.+
24 Kitu chenye kumwogopesha mwovu—hicho ndicho kitakachompata;+ lakini tamaa ya mwadilifu itatimizwa.+
25 Kama wakati upepo wa dhoruba unapopita, ndivyo na mwovu asivyokuwapo tena;+ lakini mwadilifu ni msingi mpaka wakati usio na kipimo.+
26 Kama siki kwenye meno na kama moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mtu mvivu kwa wale wanaomtuma.+
27 Kumwogopa Yehova kutaongeza siku,+ lakini miaka ya waovu itafupishwa.+
28 Tarajio la waadilifu ni kushangilia,+ lakini tumaini lenyewe la waovu litapotea.+
29 Njia ya Yehova ni ngome kwa mtu asiye na lawama,+ lakini wale wanaozoea kutenda mambo yenye kuumiza wataharibiwa.+
30 Naye mwadilifu, mpaka wakati usio na kipimo hatafanywa apepesuke,+ lakini waovu, hawataendelea kukaa duniani.+
31 Kinywa cha mwadilifu—hicho huzaa tunda la hekima,+ lakini ulimi wa upotovu utakatiliwa mbali.+
32 Midomo ya mwadilifu—hiyo hujua nia njema,+ lakini kinywa cha waovu ni upotovu.+