2 Samweli 1:1-27

1  Na ikawa baada ya kifo cha Sauli, na wakati Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwapiga Waamaleki,+ kwamba Daudi akaendelea kukaa siku mbili katika Siklagi.+  Na ikawa kwamba katika siku ya tatu, tazama! mtu+ fulani alikuwa anakuja kutoka katika kambi, kutoka kwa Sauli, mavazi yake yakiwa yameraruliwa+ na mavumbi yakiwa juu ya kichwa chake;+ na ikawa alipomjia Daudi, akaanguka chini+ mara moja na kulala kifudifudi.  Naye Daudi akamwambia: “Umetoka wapi?” naye akamjibu: “Nimekimbia kutoka katika kambi ya Israeli.”  Na Daudi akaendelea kumwambia: “Mambo yaliendaje? Niambie tafadhali.” Naye akasema: “Watu wamekimbia kutoka vitani na pia watu wengi wameanguka, wakafa,+ na hata Sauli+ na Yonathani+ mwana wake wamekufa pia.”  Kisha Daudi akamuuliza yule kijana aliyekuwa akimpasha habari: “Unajuaje hakika kwamba Sauli amekufa, na pia Yonathani mwana wake?”+  Ndipo yule kijana aliyekuwa akimpasha habari akasema: “Nilijikuta katika Mlima Gilboa+ bila kutazamia, na tazama, Sauli alikuwa amejiegemeza kwenye mkuki wake;+ na tazama! waendesha-magari na wapanda-farasi walikuwa wamemfikia.+  Alipogeuka nyuma na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Mimi hapa!’  Naye akaendelea kuniambia, ‘Wewe ni nani?’ nami nikamwambia, ‘Mimi ni Mwamaleki.’+  Kisha akasema, ‘Tafadhali, simama juu yangu, na kwa hakika uniue, kwa maana ganzi imenishika, kwa sababu nafsi+ yangu yote ingali ndani yangu.’ 10  Basi nikasimama juu yake na kwa hakika nikamuua,+ kwa maana nilijua kwamba hangeishi baada ya kuanguka. Kisha nikachukua taji+ lililokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa kwenye mkono wake, ili nivilete kwa bwana wangu hapa.” 11  Ndipo Daudi akashika mavazi yake akayararua,+ na pia watu wote waliokuwa pamoja naye wakafanya hivyo. 12  Nao wakaanza kuomboleza na kulia+ na kufunga+ mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na kwa ajili ya Yonathani mwana wake na kwa ajili ya watu wa Yehova na kwa ajili ya nyumba ya Israeli,+ kwa sababu walikuwa wameanguka kwa upanga. 13  Basi Daudi akamwambia yule kijana aliyekuwa akimpasha habari: “Unatoka wapi wewe?” naye akajibu: “Mimi ni mwana wa mkaaji mgeni, Mwamaleki.”+ 14  Kisha Daudi akamwambia: “Kwa nini hukuogopa+ kunyoosha mkono wako umwangamize mtiwa-mafuta+ wa Yehova?” 15  Kwa hiyo Daudi akamwita mmoja wa vijana na kumwambia: “Sogea karibu. Mpige.” Basi akampiga, naye akafa.+ 16  Ndipo Daudi akamwambia: “Hatia yako ya damu na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe,+ kwa sababu kinywa chako mwenyewe kimetoa ushuhuda juu yako,+ kusema, ‘Mimi mwenyewe kwa hakika nilimuua mtiwa-mafuta wa Yehova.’”+ 17  Na Daudi akaimba wimbo huu wa huzuni+ kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwana wake+ 18  na kusema kwamba wana wa Yuda+ wafundishwe “Upinde.”+ Tazama! Umeandikwa katika kitabu cha Yashari:+ 19  “Ee Israeli, uzuri umeuawa katika mahali pako pa juu.+Lo! Jinsi walivyoanguka wanaume wenye nguvu! 20  Msiseme hayo katika Gathi;+Msiyatangaze katika barabara za Ashkeloni,+Binti za Wafilisti wasije wakashangilia,Binti za watu wasiotahiriwa wasije wakafurahi.+ 21  Enyi milima ya Gilboa,+ umande wowote, wala mvua yoyote isinyeshe juu yenu, wala kusiwe na mashamba ya michango mitakatifu;+Kwa sababu ngao ya wenye uwezo ilichafuliwa hapo,Ngao ya Sauli, hata kukawa hakuna yoyote iliyotiwa mafuta.+ 22  Kutoka kwa damu ya waliouawa, kutoka kwa mafuta ya wenye uwezo,Upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma,+Na upanga wa Sauli haukurudi bila mafanikio.+ 23  Sauli na Yonathani,+ watu wenye kupendwa na wenye kupendeza wakati wa maisha yao,Nao hawakutenganishwa katika kifo chao.+Walikuwa wepesi kuliko tai,+Walikuwa wenye nguvu kuliko simba.+ 24  Enyi binti za Israeli, mlilieni Sauli,Aliyewavika nguo nyekundu kwa umaridadi,Aliyeweka mapambo ya dhahabu juu ya mavazi yenu.+ 25  Lo! Jinsi wenye nguvu walivyoanguka katikati ya pigano!+Yonathani ameuawa juu ya mahali pako pa juu!+ 26  Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu,Ulinipendeza sana.+Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu sana kuliko upendo kutoka kwa wanawake.+ 27  Lo! Jinsi wenye uwezo walivyoanguka+Na silaha za vita kuangamia!”

Maelezo ya Chini