2 Samweli 1:1-27
1 Na ikawa baada ya kifo cha Sauli, na wakati Daudi alipokuwa amerudi kutoka kuwapiga Waamaleki,+ kwamba Daudi akaendelea kukaa siku mbili katika Siklagi.+
2 Na ikawa kwamba katika siku ya tatu, tazama! mtu+ fulani alikuwa anakuja kutoka katika kambi, kutoka kwa Sauli, mavazi yake yakiwa yameraruliwa+ na mavumbi yakiwa juu ya kichwa chake;+ na ikawa alipomjia Daudi, akaanguka chini+ mara moja na kulala kifudifudi.
3 Naye Daudi akamwambia: “Umetoka wapi?” naye akamjibu: “Nimekimbia kutoka katika kambi ya Israeli.”
4 Na Daudi akaendelea kumwambia: “Mambo yaliendaje? Niambie tafadhali.” Naye akasema: “Watu wamekimbia kutoka vitani na pia watu wengi wameanguka, wakafa,+ na hata Sauli+ na Yonathani+ mwana wake wamekufa pia.”
5 Kisha Daudi akamuuliza yule kijana aliyekuwa akimpasha habari: “Unajuaje hakika kwamba Sauli amekufa, na pia Yonathani mwana wake?”+
6 Ndipo yule kijana aliyekuwa akimpasha habari akasema: “Nilijikuta katika Mlima Gilboa+ bila kutazamia, na tazama, Sauli alikuwa amejiegemeza kwenye mkuki wake;+ na tazama! waendesha-magari na wapanda-farasi walikuwa wamemfikia.+
7 Alipogeuka nyuma na kuniona, akaniita, nami nikasema, ‘Mimi hapa!’
8 Naye akaendelea kuniambia, ‘Wewe ni nani?’ nami nikamwambia, ‘Mimi ni Mwamaleki.’+
9 Kisha akasema, ‘Tafadhali, simama juu yangu, na kwa hakika uniue, kwa maana ganzi imenishika, kwa sababu nafsi+ yangu yote ingali ndani yangu.’
10 Basi nikasimama juu yake na kwa hakika nikamuua,+ kwa maana nilijua kwamba hangeishi baada ya kuanguka. Kisha nikachukua taji+ lililokuwa juu ya kichwa chake na kikuku kilichokuwa kwenye mkono wake, ili nivilete kwa bwana wangu hapa.”
11 Ndipo Daudi akashika mavazi yake akayararua,+ na pia watu wote waliokuwa pamoja naye wakafanya hivyo.
12 Nao wakaanza kuomboleza na kulia+ na kufunga+ mpaka jioni kwa ajili ya Sauli na kwa ajili ya Yonathani mwana wake na kwa ajili ya watu wa Yehova na kwa ajili ya nyumba ya Israeli,+ kwa sababu walikuwa wameanguka kwa upanga.
13 Basi Daudi akamwambia yule kijana aliyekuwa akimpasha habari: “Unatoka wapi wewe?” naye akajibu: “Mimi ni mwana wa mkaaji mgeni, Mwamaleki.”+
14 Kisha Daudi akamwambia: “Kwa nini hukuogopa+ kunyoosha mkono wako umwangamize mtiwa-mafuta+ wa Yehova?”
15 Kwa hiyo Daudi akamwita mmoja wa vijana na kumwambia: “Sogea karibu. Mpige.” Basi akampiga, naye akafa.+
16 Ndipo Daudi akamwambia: “Hatia yako ya damu na iwe juu ya kichwa chako mwenyewe,+ kwa sababu kinywa chako mwenyewe kimetoa ushuhuda juu yako,+ kusema, ‘Mimi mwenyewe kwa hakika nilimuua mtiwa-mafuta wa Yehova.’”+
17 Na Daudi akaimba wimbo huu wa huzuni+ kwa ajili ya Sauli na Yonathani mwana wake+
18 na kusema kwamba wana wa Yuda+ wafundishwe “Upinde.”+ Tazama! Umeandikwa katika kitabu cha Yashari:+
19 “Ee Israeli, uzuri umeuawa katika mahali pako pa juu.+Lo! Jinsi walivyoanguka wanaume wenye nguvu!
20 Msiseme hayo katika Gathi;+Msiyatangaze katika barabara za Ashkeloni,+Binti za Wafilisti wasije wakashangilia,Binti za watu wasiotahiriwa wasije wakafurahi.+
21 Enyi milima ya Gilboa,+ umande wowote, wala mvua yoyote isinyeshe juu yenu, wala kusiwe na mashamba ya michango mitakatifu;+Kwa sababu ngao ya wenye uwezo ilichafuliwa hapo,Ngao ya Sauli, hata kukawa hakuna yoyote iliyotiwa mafuta.+
22 Kutoka kwa damu ya waliouawa, kutoka kwa mafuta ya wenye uwezo,Upinde wa Yonathani haukugeuka nyuma,+Na upanga wa Sauli haukurudi bila mafanikio.+
23 Sauli na Yonathani,+ watu wenye kupendwa na wenye kupendeza wakati wa maisha yao,Nao hawakutenganishwa katika kifo chao.+Walikuwa wepesi kuliko tai,+Walikuwa wenye nguvu kuliko simba.+
24 Enyi binti za Israeli, mlilieni Sauli,Aliyewavika nguo nyekundu kwa umaridadi,Aliyeweka mapambo ya dhahabu juu ya mavazi yenu.+
25 Lo! Jinsi wenye nguvu walivyoanguka katikati ya pigano!+Yonathani ameuawa juu ya mahali pako pa juu!+
26 Nimesikitika kwa ajili yako, Yonathani ndugu yangu,Ulinipendeza sana.+Upendo wako kwangu ulikuwa wa ajabu sana kuliko upendo kutoka kwa wanawake.+
27 Lo! Jinsi wenye uwezo walivyoanguka+Na silaha za vita kuangamia!”