1 Yohana 4:1-21

4  Wapendwa, msiamini kila neno lililoongozwa na roho,+ lakini yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ili kuona kama yanatokana na Mungu,+ kwa sababu manabii wengi wa uwongo wameingia ulimwenguni.+  Mnalijua neno lililoongozwa na roho kutoka kwa Mungu+ kwa njia hii: Kila neno lililoongozwa na roho linalomkiri Yesu Kristo kuwa alikuja katika mwili hutokana na Mungu,+  lakini kila neno lililoongozwa na roho ambalo halimkiri Yesu halitokani na Mungu.+ Zaidi ya hayo, hili ndilo neno lililoongozwa na roho la yule mpinga-Kristo ambalo mmesikia kwamba linakuja,+ na sasa tayari limo ulimwenguni.+  Ninyi mnatokana na Mungu, watoto wadogo, nanyi mmewashinda watu hao,+ kwa sababu yeye aliye katika muungano+ na ninyi ni mkuu+ kuliko yeye aliye katika muungano na ulimwengu.+  Wao hutokana na ulimwengu;+ ndiyo sababu wanasema lile linalotoka kwa ulimwengu na ulimwengu huwasikiliza wao.+  Sisi tunatokana na Mungu.+ Yeye ambaye anamjua Mungu hutusikiliza;+ yeye ambaye hatokani na Mungu hatusikilizi.+ Hivi ndivyo tunavyojua neno la kweli lililoongozwa na roho na neno lenye kosa lililoongozwa na roho.+  Wapendwa, acheni tuendelee kupendana,+ kwa sababu upendo+ unatoka kwa Mungu, na kila mtu ambaye hupenda amezaliwa kutokana na Mungu+ na hupata kumjua Mungu.+  Yeye ambaye hapendi hajamjua Mungu, kwa sababu Mungu ni upendo.+  Kwa hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwa habari yetu,+ kwa sababu Mungu alimtuma Mwana+ wake mzaliwa-pekee kuja ulimwenguni ili tupate uzima kupitia yeye.+ 10  Hivi ndivyo upendo ulivyo, si kwamba sisi tumempenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda akamtuma Mwana wake kuwa dhabihu+ ya upatanisho+ kwa ajili ya dhambi zetu.+ 11  Wapendwa, ikiwa Mungu alitupenda hivi, basi sisi wenyewe tuko chini ya wajibu wa kupendana.+ 12  Hakuna yeyote ambaye amemwona Mungu wakati wowote.+ Tukiendelea kupendana, Mungu hukaa ndani yetu na upendo wake unakamilishwa ndani yetu.+ 13  Kwa hili sisi tunajua kwamba tunakaa katika muungano+ na yeye na yeye katika muungano na sisi,+ kwa sababu ametupa sisi roho yake.+ 14  Kwa kuongezea, sisi wenyewe tumemwona+ na tunatoa ushahidi+ kwamba Baba amemtuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa ulimwengu.+ 15  Yeyote anayekiri kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu,+ Mungu hukaa katika muungano na mtu huyo na yeye katika muungano na Mungu.+ 16  Na sisi wenyewe tumejua na tumeamini upendo+ ambao Mungu anao kwa habari yetu. Mungu ni upendo,+ na yeye ambaye hukaa katika upendo+ hukaa katika muungano na Mungu na Mungu hukaa katika muungano+ na yeye. 17  Hivi ndivyo upendo umekamilishwa ndani yetu, kwamba tuwe na uhuru wa kusema+ katika siku ya hukumu,+ kwa sababu, kama vile huyo alivyo, ndivyo tulivyo sisi wenyewe katika ulimwengu huu.+ 18  Hakuna woga katika upendo,+ lakini upendo mkamilifu hutupa woga nje,+ kwa sababu woga hutokeza kizuizi. Kwa kweli, yeye ambaye yuko chini ya woga hajakamilishwa katika upendo.+ 19  Kwa habari yetu, sisi tunaonyesha upendo, kwa sababu yeye alitupenda sisi kwanza.+ 20  Yeyote akisema: “Mimi nampenda Mungu,” na bado anamchukia ndugu yake, yeye ni mwongo.+ Kwa maana yeye ambaye hampendi ndugu yake,+ ambaye amemwona, hawezi kuwa anampenda Mungu, ambaye hajamwona.+ 21  Na amri hii tunayo kutoka kwake,+ kwamba yeye ambaye anampenda Mungu anapaswa kuwa akimpenda ndugu yake pia.+

Maelezo ya Chini