Hamia kwenye habari

Safu ya juu (kushoto hadi kulia): Ndugu Nikolay Anufriyev; Ndugu Eduard Merinkov na mke wake, Valentina; Ndugu Gennadiy Polyakevich; na Ndugu Aleksandr Prilepskiy

Safu ya chini (kushoto hadi kulia): Ndugu Viktor Shchannikov na mke wake, Viktoria; Ndugu Gennadiy Skutelets; na Ndugu Aleksandr Vorontsov na mke wake, Yelena

JANUARI 20, 2022 | HABARI ZIMEONGEZWA: DESEMBA 19, 2024
URUSI

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WAPIGWA FAINI | Ndugu Saba Nchini Urusi Wanamtegemea Yehova Anayewapa Nguvu

HABARI ZA KARIBUNI—NDUGU WAPIGWA FAINI | Ndugu Saba Nchini Urusi Wanamtegemea Yehova Anayewapa Nguvu

Desemba 17, 2024, Mahakama ya Jiji la Pechora katika Jamhuri ya Komi iliwahukumu Ndugu Nikolay Anufriyev, Ndugu Eduard Merinkov, Ndugu Gennadiy Polyakevich, Ndugu Aleksandr Prilepskiy, Ndugu Viktor Shchannikov, Ndugu Gennadiy Skutelets, na Ndugu Aleksandr Vorontsov. Ndugu sita kati yao walitozwa faini. Nikolay, Eduard, Viktor, na Aleksandr Vorontsov walitozwa faini ya rubo 600,000 (dola 5,797.00 za Marekani); Gennadiy Skutelets alitozwa faini ya rubo 250,000 (dola 2,413.00 za Marekani); na Gennadiy Polyakevich alitozwa faini ya rubo 200,000 (dola 1,931.00 za Marekani). Aleksandr Prilepskiy alihukumiwa kuwa na hatia, lakini kesi hiyo ilifutiliwa baada ya kifo chake mwezi Desemba 2022.

Mfuatano wa Matukio

  1. Januari 28, 2020

    Wenye mamlaka walifanya msako katika nyumba za familia 12 za Mashahidi wa Yehova katika Jamhuri ya Komi. Kesi ya uhalifu dhidi ya Ndugu Polyakevich na Ndugu Skutelets ilianzishwa

  2. Januari 30, 2020

    Gennadiy Polyakevich alipelekwa mahabusu na Gennadiy Skutelets alifungwa kifungo cha nyumbani

  3. May 20-25, 2020

    Wenye mamlaka waliwahoji akina ndugu na dada wengine kutoka Pechora ili waone ikiwa wangewatumia kama mashahidi katika kesi hiyo ya uhalifu. Ndugu mmoja alipatwa na ugonjwa wa kiharusi baada ya kutishwa na mpelelezi mmoja. Sasa amepata nafuu

  4. Juni 26, 2020

    Muda wa Gennadiy Polyakevich kukaa mahabusu uliongezwa. Hakimu alisema kwamba Gennadiy Polyakevich anashtakiwa kwa “kutenda kimakusudi uhalifu mkubwa,” unaotia ndani kuzungumza kuhusu “umuhimu wa kuendelea kumtumikia Yehova licha ya kuteswa na wenye mamlaka.”

  5. Agosti 24, 2020

    Wenye mamlaka walifanya msako katika nyumba za familia nyingine 12 za Mashahidi

  6. Novemba 10, 2020

    Kesi ya uhalifu ilianzishwa dhidi ya Aleksandr Prilepskiy, Aleksandr Vorontsov, Eduard, Nikolay, na Viktor. Kesi hiyo iliunganishwa na kesi ya uhalifu dhidi ya Gennadiy Polyakevich na Gennadiy Skutelets

  7. Novemba 25, 2020

    Baada ya kukaa mahabusu siku 300, Gennadiy Polyakevich aliachiliwa kisha akafungwa kifungo cha nyumbani

  8. Januari 27, 2021

    Baada ya kuwa katika kifungo cha nyumbani kwa siku 363, Gennadiy Skutelets aliachiliwa

Maelezo Mafupi Kuwahusu

Tuna uhakika kwamba ndugu zetu walio na imani katika wema wa Yehova watabarikiwa sasa na wakati ujao pia.​—Zaburi 27:13.